Mbele sijakuja ulikuwa na mali chache tu lakini tangu nifike, mali yako imeongezeka kwa wingi sana, na Yawe amekubariki kila fasi nilikokwenda. Lakini sasa, nitatunza wakati gani jamaa yangu mwenyewe?”
Uniruhusu nipite kati ya nyama wako wote leo, nitenge katika kundi kila nyama mwenye madoadoa na matakamataka, kila nyama mweusi, kati ya kondoo na mbuzi wanaokuwa na madoadoa na matakamataka. Huo ndio utakaokuwa mushahara wangu.
Musijiachilie kutawaliwa na tamaa ya mali katika maisha yenu, lakini mutoshelewe na vitu munavyokuwa navyo, kwa maana Mungu mwenyewe amesema: “Sitakusahau wala kukuachilia.”