Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 30:30 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

30 Mbele sijakuja ulikuwa na mali chache tu lakini tangu nifike, mali yako imeongezeka kwa wingi sana, na Yawe amekubariki kila fasi nilikokwenda. Lakini sasa, nitatunza wakati gani jamaa yangu mwenyewe?”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 30:30
7 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yakobo akamwambia: “Wewe mwenyewe unajua jinsi nilivyokutumikia, na jinsi nilivyowatunza nyama wako.


Labani akamwuliza: “Nikupatie nini?” Yakobo akamujibu: “Hautanipatia kitu chochote. Nitaendelea kuwatunza nyama wako ikiwa utanifanyia jambo hili:


Basi, Yakobo akatajirika sana, akakuwa na makundi makubwa ya nyama, wajakazi na watumwa, ngamia na punda.


wakati wa kutafuta na wakati wa kupoteza, wakati wa kuchunga na wakati wa kutupa,


Sasa mimi niko tayari kufika kwenu kwa mara ya tatu, nami sitawalemea. Maana sihitaji mali yenu, lakini ninawahitaji ninyi. Kwa sababu si kazi ya watoto kuwawekea wazazi wao akiba, lakini ni kazi ya wazazi kuwawekea watoto wao akiba.


Inchi munayokwenda kurizi si kama inchi ya Misri mulikotoka, ambako mulipanda ngano nanyi mulipaswa kuleta maji kutoka kwenye mito kwa kuimwangilia kama vile mulivyofanya kwa mashamba ya mboga.


Kama mutu asipotunza wandugu zake na hasa zaidi watu wa jamaa yake mwenyewe, huyu amekana imani yake naye ni mubaya kuliko mupagani.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ