Mutumishi wa Abrahamu na watu aliokuja nao wakakula, wakakunywa na kulala kule. Walipoamuka asubui, mutumishi yule akasema: “Ninaomba kurudi kwa bwana wangu.”
Lakini yeye akasema: “Tafazali, musinicheleweshe, kwa sababu Yawe amekwisha kufanikisha katika safari yangu. Ninaomba muniruhusu kurudi kwa bwana wangu.”
Ukae katika inchi hiyo, nami nitakuwa pamoja nawe na kukubariki. Nitatimiza ahadi niliyomupa baba yako Abrahamu, maana nitakupa wewe na wazao wako inchi hizi zote.
Yawe alisimama juu ya ngazi hiyo, akamwambia: “Mimi ni Yawe, Mungu wa Abrahamu baba yako, na Mungu wa Isaka. Nitakupa inchi unayoilalia wewe na wazao wako.
Mimi ndimi yule Mungu aliyekutokea kule Beteli, pahali pale ulipotakasa lile jiwe kwa kulimiminia mafuta na ambapo ulifanyia kiapo. Sasa ondoka katika inchi hii urudi katika inchi yako.’ ”
Kwa njia ya imani, aliishi kama vile mugeni katika inchi ile Mungu aliyomwahidi. Yeye alikuwa akiishi katika hema kama vile Isaka na Yakobo walivyoishi. Wao vilevile walishiriki pamoja naye ahadi ile ile ya Mungu.