Hizi ndizo habari za ukoo wa Yakobo. Yosefu, akiwa kijana wa umri wa miaka kumi na saba, alikuwa akichunga kondoo na mbuzi pamoja na wandugu zake, wana wa Biliha na Zilpa, wake za baba yake. Yosefu akakuwa anamujulisha baba yake juu ya tabia mbaya za wandugu zake.
Wakati ule Yosefu alikuwa mukubwa kule Misri. Yeye ndiye aliyekuwa akiwauzishia wanainchi ngano. Basi, kaka zake wakakuja na kuinama mbele ya Yosefu kwa heshima.
Wewe mwanadamu, twaa kijiti kimoja, uandike juu yake maneno haya: Kwa Yuda na Waisraeli wanaoshirikiana naye. Kisha twaa kijiti kingine uandike juu yake maneno haya: Kwa Yosefu (kijiti cha Efuraimu) na Waisraeli wanaoshirikiana naye.