Basi, Sarai akamwambia Abramu: “Unajua kwamba Yawe hajanijalia kupata watoto. Umutwae Hagari mujakazi wangu. Labda nitapata watoto kutoka kwake.” Abramu akakubali shauri la Sarai.
Mufalme wa Israeli aliposoma barua hii alipasua nguo yake na kusema: “Sababu gani mufalme wa Aramu anataka nimuponyeshe mutu huyu ukoma wake? Anafikiri kwamba mimi ni Mungu anayekuwa na uwezo wa kuua au kufufua? Mufahamu basi, muone kwamba mutu huyu anataka kuniletea ugomvi!”
Mara tu walipokaribia kambi walimwona yule mwana-ngombe na watu wakicheza. Hapo hasira ya Musa ikawaka kama moto, akatupa chini vile vibao kutoka mikono yake na kuvivunja pale chini ya mulima.
Yesu akawakazia macho kwa kasirani, akihuzunika kwa sababu ya ugumu wao. Akamwambia yule mutu: “Nyoosha mukono wako.” Akaunyoosha, nao ukakuwa muzima tena.