Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 3:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Mungu alisema hivyo kwa sababu anajua kwamba mukikula matunda ya muti ule mutafumbuliwa macho, nanyi mutakuwa kama Mungu, mukijua mazuri na mabaya.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 3:5
31 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini usikule matunda ya muti wa kujua mazuri na mabaya, maana siku utakapokula matunda ya muti ule, hakika utakufa.”


Yawe Mungu akaotesha kutoka udongo kila aina ya miti ya kupendeza macho na inayofaa kwa chakula. Katikati ya bustani hiyo kulikuwa muti wa uzima na muti wa kujua mazuri na mabaya.


Naye akamujibu: “Nilisikia sauti yako katika bustani, nikaogopa maana nilikuwa uchi. Nikajificha.”


Kisha Yawe Mungu akasema: “Sasa, mwanadamu amekuwa kama mumoja wetu, anajua mazuri na mabaya. Inafaa kumuzuia kula lile tunda la muti wa uzima, maana akilikula ataishi milele.”


Mara moja macho yao yakafumbuliwa, wakatambua kwamba wako uchi. Kwa hiyo wakashona majani ya muti wa tini, wakajifanyia nguo.


Basi, Ahabu akakusanya manabii yapata mia ine, akawauliza: “Niende au nisiende kushambulia Ramoti-Gileadi?” Nao wakamujibu: “Kwenda! Yawe atakupatia ushindi.”


Musidanganywe na Hezekia wala musishawishiwe kwa hayo. Musimwamini mutu huyu, kwa maana hakujatokea mungu wa taifa au mufalme yeyote aliyeweza kuwakomboa watu wake kutoka mikono ya mufalme wa Asuria. Vile vile mungu wenu hataweza!”


Ee Yawe, ukomeshe midomo hiyo ya kudanganya, na ndimi hizo zinazojigamba.


Usitaje bure jina langu mimi Yawe, Mungu wako, maana mimi Yawe sitaacha kumwazibu yeyote anayetaja bure jina langu.


Lakini mufalme wa Misri akawauliza: “Ni nani yule Yawe, hata nimusikilize na kuwaacha Waisraeli waondoke? Mimi simujui yule Yawe, wala sitawaruhusu Waisraeli waondoke.”


Nitapanda juu ya mawingu nitajifanya kuwa sawa na Mungu Mukubwa.


Kwa sababu mumewavunja watu wa haki moyo kwa kusema uongo, ijapokuwa mimi sikuwavunja moyo, mukawaimarisha waovu wasiache mienendo yao mibaya na kuokoa maisha yao,


Wewe mwanadamu! Imba wimbo wa maombolezo juu ya mufalme wa Tiro. Umwambie kwamba: Bwana wetu Yawe anasema hivi: Wewe mufalme wa Tiro ulikuwa mupaka wa ukamilifu; ulijaa hekima na uzuri kamili.


Wewe mwanadamu! Umwambie mufalme wa Tiro kwamba Bwana wenu Yawe anasema hivi: Wewe una kiburi cha moyo, na umesema kwamba wewe ni mungu, kwamba umeikalia kiti cha kifalme cha miungu, umekaa mbali huko katika bahari. Lakini, wewe ni mutu tu wala si mungu, ingawa unajiona kuwa na hekima kama mungu.


Utaendelea kujiona kuwa mungu mbele ya hao watakaokuua? Katika mikono ya hao watakaokuangamiza, utatambua kwamba wewe ni mutu tu, wala si mungu!


Umwambie kwamba Bwana wetu Yawe anasema hivi: Mimi nitapingana na wewe mufalme wa Misri, wewe mamba unayelala ndani ya muto Nili! Wewe unafikiri kwamba muto Nili ni wako, kwamba wewe ndiwe uliyeufanya!


Mara moja jambo hilo juu ya mufalme Nebukadneza likatimizwa. Alifukuzwa mbali na wanadamu, akakuwa anakula majani kama ngombe. Alilowanishwa na umande wa mbinguni, na nywele zake zikakuwa ndefu kama manyoya ya tai, na kucha zake kama za ndege.


Basi, hao wakubwa na maliwali wote pamoja, wakamwendea mufalme na kumwambia: Uishi milele ee mufalme Dario!


Lakini kama macho yako yanaharibika, mwili wako wote utabaki katika giza. Basi ikiwa mwangaza unaokuwa ndani yako umegeuka kuwa giza, giza hilo ni nzito sana!


kusudi ufungue macho yao, ukiwaongoza watoke katika giza na kuwaingiza katika mwangaza. Watatoka chini ya uwezo wa Shetani na kumugeukia Mungu, kusudi kwa njia ya kuniamini wapate kusamehewa zambi zao na kupewa urizi pamoja na watu wake watakatifu.’


Lakini ninaogopa kwamba sawa vile nyoka alivyomudanganya Eva kwa werevu wake, mawazo yenu vilevile yasipotoshwe hata mupate kupoteza uaminifu na ukamilifu wenu kwa Kristo.


Wao hawaamini kwa sababu yule mungu wa dunia hii amefunika akili zao. Yeye anawazuiza wasione mwangaza unaoletwa na Habari Njema ya utukufu wa Kristo, anayefanana na Mungu.


Yeye atapinga kitu chochote watu wanachohesabu kuwa cha kimungu au wanachoabudu na kujiweka kuwa juu ya vyote. Yeye ataenda hata kuingia katika hekalu la Mungu na kukaa mule na kujiita mwenyewe kuwa Mungu.


Akawadanganya wakaaji wa dunia kwa njia ya vitambulisho alivyowezeshwa kuonyesha mbele ya yule nyama mukubwa wa kwanza. Aliwaambia watu wa dunia watengeneze sanamu kwa heshima ya yule nyama aliyeumizwa kwa upanga, lakini aliendelea kuishi.


Nao wakaanza kumwabudu yule nyoka kwa sababu alimupa yule nyama uwezo wake. Vilevile wakamwabudu yule nyama, wakisema: “Ni nani anayefanana na nyama huyu? Ni nani anayeweza kupigana vita naye?”


Alifanya hivyo kusudi awape watu wa vizazi hivyo ujuzi wa kupigana maana hawakukuwa wameona vita.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ