Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 3:24 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

24 Alimufukuza inje. Akaweka makerubi upande wa mashariki wa bustani ya Edeni wakiwa na upanga wa moto uliogeuka huku na kule, kwa kulinda njia inayokwenda kwenye muti wa uzima.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 3:24
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, Yawe Mungu akamufukuza Adamu inje ya bustani ya Edeni, kusudi alime udongo ambamo alitwaliwa.


Adamu akalala na muke wake Eva, naye akapata mimba, akazaa Kaina. Eva akasema: “Nimepata mutoto mwanaume kwa musaada wa Yawe!”


Angalia, leo umenifukuza kutoka udongo wenye mboleo na mbali nawe. Basi, nitakuwa mukimbizi na mwenye kutangatanga katika dunia, na yeyote atakayeniona ataniua.”


Unaufanya upepo kuwa mujumbe wako, moto na ndimi zake kuwa watumishi wako.


Kwa mukubwa wa waimbaji. Kwa mutindo wa wimbo. Zaburi ya Asafu.


Yawe anatawala, mataifa yanatetemeka! Ameikaa juu ya makerubi, nayo dunia inatikisika!


Uwaambie Waisraeli wanipe michango ya matoleo. Utapokea matoleo kutoka kwa mutu yeyote atakayetoa kwa moyo safi.


Kisha nikaona kwamba katika lile anga juu ya vichwa vya makerubi kulikuwa kitu kinachofanana na jiwe la rangi ya samawi, umbo lake kama kiti cha kifalme.


nitautia katika mikono ya mukubwa kati ya mataifa. Yeye, atauazibu. Nimeutupilia mbali kadiri ya uovu wake.


Basi, punda akamwona malaika huyo wa Yawe amesimama katika njia, akishika upanga uliochomolewa. Kwa hiyo akaacha njia, akaenda pembeni. Balamu akamupiga huyo punda, akamurudisha katika njia.


Yesu akamujibu: “Mimi ni njia, ukweli na uzima. Mutu hawezi kufika kwa Baba asipopitia kwangu.


Lakini juu ya wamalaika, Mungu alisema: “Mungu anawafanya wamalaika wake kuwa kama upepo. Anawafanya hao watumishi wake kuwa kama ndimi za moto.”


Siku moja Yoshua alipokuwa karibu na muji wa Yeriko, aliona kwa rafla mutu mumoja akisimama mbele yake na upanga uliochomolewa katika mukono wake. Yoshua akamwendea, akamwuliza: “Wewe ni wetu au ni wa waadui zetu?”


Kwa hiyo, walituma watumishi kule Shilo, nao wakalileta Sanduku la Agano la Yawe wa majeshi ambaye anatawala juu ya makerubi. Wale wana wawili wa Eli, Hofuni na Finehasi walikuja pamoja na lile Sanduku la Agano la Mungu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ