Kisha Yawe Mungu akasema: “Sasa, mwanadamu amekuwa kama mumoja wetu, anajua mazuri na mabaya. Inafaa kumuzuia kula lile tunda la muti wa uzima, maana akilikula ataishi milele.”
Alimufukuza inje. Akaweka makerubi upande wa mashariki wa bustani ya Edeni wakiwa na upanga wa moto uliogeuka huku na kule, kwa kulinda njia inayokwenda kwenye muti wa uzima.