Kisha akamwambia yule mwanaume: “Wewe umemusikiliza muke wako na kula matunda ya muti ambayo nilikuamuru usikule. Basi, udongo umelaaniwa kwa sababu yako. Kwa jasho utajipatia toka humo chakula chako, siku zote za maisha yako.
Nitalifanya ukiwa kabisa, mizabibu yake haitasafishwa matawi wala kupaliliwa. Litaota michongoma na miiba. Tena nitayaamuru mawingu yasinyeshe mvua juu yake.
Kwa mufano, mutu mumoja kutokana na imani yake anaona kwamba anaweza kula kila chakula, lakini mwingine kutokana na imani yake zaifu, anakula tu mboga za majani.
mujue kwa hakika kwamba Yawe, Mungu wenu, hataendelea kuyafukuza mataifa haya mbele yenu, lakini yatakuwa kwenu kikwazo na mutego. Yatakuwa kwenu mujeledi wa kuwapiga na miiba ya kuwachoma kwa macho mpaka pale mutakapoangamia na kutoka katika inchi hii nzuri ambayo Yawe, Mungu wenu, amewapa.