Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 3:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Naye akamujibu: “Nilisikia sauti yako katika bustani, nikaogopa maana nilikuwa uchi. Nikajificha.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 3:10
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Huyo mwanaume na muke wake wote walikuwa uchi, lakini hawakuona haya.


Yawe akamwuliza: “Nani aliyekuambia kwamba uko uchi? Umekula tunda la muti nililokuamuru usikule?”


Mara moja macho yao yakafumbuliwa, wakatambua kwamba wako uchi. Kwa hiyo wakashona majani ya muti wa tini, wakajifanyia nguo.


Kwa hivyo, ninatetemeka kwa hofu mbele yake; hata nikifikiri tu ninapatwa na woga.


Nimeficha makosa yangu kama wengine? Nimekataa kutambua zambi zangu?


Ninatetemeka kwa kukuogopa wewe; nimejaa hofu kwa sababu ya maamuzi yako.


Watu waliposikia ngurumo na kuona umeme ukiwaka na kusikia sauti ya baragumu juu ya mulima uliokuwa unafuka moshi, wote wakaogopa na kutetemeka. Wote wakasimama mbali,


wakamwambia Musa: Sema nasi wewe mwenyewe, nasi tutakusikiliza. Lakini Yawe asiseme nasi, tusikufe.


Kisha Mungu akamwambia: “Mimi ni Mungu wa baba yako, Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo.” Musa akafunika uso wake kwa sababu aliogopa kumwangalia Mungu.


Basi, Musa alipoona kwamba watu wameasi na kufanya wanavyopenda (kwa kuwa Haruni aliwafanya waasi na kufanya wanavyopenda na kujiletea haya mbele ya waadui zao),


Wenye zambi katika Sayuni wanaogopa, wasiomwamini Mungu wanatetemeka na kusema: Nani anayeweza kuvumilia moto huu mukali? Nani anayeweza kuvumilia ndimi za moto usiozimika?


Watu watauona uchi wako; wataona haya yako. Mimi nitalipiza kisasi, wala sitamuhurumia mutu yeyote.


Mulimwogopa na kutishwa na nani hata mukasema uongo, mukaacha kunikumbuka mimi na kuacha kabisa kufikiri juu yangu? Mimi sikuwaambia kitu kwa muda murefu; ndiyo maana labda mukaacha kuniheshimu!


Lakini kwa nini kujitia katika hatari ya kufa kwa kuteketezwa na ule moto mukubwa? Tukisikia tena sauti ya Yawe, Mungu wetu tutakufa!


Kwa maana hata kama zamiri yetu inatuhukumu, tunajua kwamba mafikiri ya Mungu yanapita zamiri yetu, naye anajua yote.


“Sikiliza, ninakuja kwa saa isiyozaniwa kama vile mwizi. Heri yule anayekesha na kutunza nguo zake vizuri kusudi asitembee uchi na kujifezehesha mbele ya watu.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ