Tera akatwaa Abramu mwana wake, Loti mujukuu wake aliyekuwa mwana wa Harani, na Sarai muke wa Abramu, wakaondoka wote pamoja toka Uri, muji wa Wakaldea, na kwenda katika inchi ya Kanana. Lakini walipofika Harani, wakakaa pale.
Kisha, yule mutumishi akatwaa ngamia kumi wa bwana wake akaondoka akiwa na zawadi nzuri za kila aina. Akasafiri kwenda katika muji Nahori alimokaa, katika inchi ya Mesopotamia.
Kwa kawaida, makundi yote ya kondoo yalipokusanyika, wachungaji walirudisha lile jiwe kwa pamoja toka kwenye kisima na kuwakunywesha kondoo. Halafu walifunika tena kisima kwa jiwe lile.
Stefano akamujibu: “Wandugu zangu na wababa zangu, munisikilize! Mungu mwenye utukufu alimutokea babu yetu mukubwa Abrahamu wakati alipokuwa angali katika inchi ya Mesopotamia, mbele hajahamia katika muji Harani.
Basi Abrahamu akatoka katika inchi ya Wababeli akaenda kukaa Harani. Kisha kufa kwa baba yake, Mungu akamuhamisha tena, akakuja kukaa katika inchi hii munayoishi ndani yake sasa.