6 Esau akatambua kwamba Isaka alibariki Yakobo na kumutuma aende kuoa kule Padani-Aramu, na kwamba alipomubariki, alimukataza asioe mwanamuke Mukanana.
Isaka alipokuwa na umri wa miaka makumi ine akamwoa Rebeka, binti ya Betueli, Musuria wa Padani-Aramu. Rebeka alikuwa dada ya Labani.
Hapo Isaka akatetemeka sana, akasema: “Ni nani basi yule aliyewinda na kuniletea nyama ya mawindo, nami nimekwisha kula mbele haujakuja? Tena nimekwisha kumubariki. Hakika, amekwisha kubarikiwa!”
Hivyo Isaka akamwita Yakobo, akamubariki, akamwagiza akisema: “Usioe mwanamuke yeyote Mukanana.
Akatambua vilevile kwamba Yakobo alimutii mama yake na baba yake, akakwenda Padani-Aramu.