Mwanzo 28:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
4 Akubariki wewe pamoja na wazao wako kama alivyomubariki Abrahamu, upate kurizi inchi ambamo unakaa kama mugeni, inchi ambayo Mungu alimupa Abrahamu!”
Sisi tuko wageni mbele yako, na wasafiri kama vile babu zetu walivyokuwa wote. Siku zetu katika dunia ni kama kivuli kinachopita, hapa hakuna tumaini la kukaa.
Ilitendeka hivi kusudi kwa njia ya Yesu Kristo, baraka Mungu aliyoahidi kwa Abrahamu itolewe vilevile kwa watu wa mataifa mengine na hata sisi kwa njia ya imani, tupate kupokea yule Roho aliyeahidiwa na Mungu.
Vilevile Maandiko Matakatifu yalisema tangu zamani kwamba watu wa mataifa mengine watahesabiwa haki mbele ya Mungu kwa njia ya imani yao. Kwa sababu Mungu alipasha kwanza Habari Njema hii kwa Abrahamu: “Kwa njia yako mataifa yote yatabarikiwa.”
Asifiwe Mungu, Baba ya Bwana wetu Yesu Kristo! Yeye ndiye aliyetupatia baraka za kiroho za kila namna kutoka katika eneo la mbingu kwa njia ya kuungana kwetu na Kristo.