Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 28:21 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

21 kusudi nirudi katika nyumba ya baba yangu salama, basi, wewe Yawe utakuwa ndiwe Mungu wangu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 28:21
8 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Maana, mimi mutumishi wako, nilipoishi kule Gesuri katika inchi ya Aramu, nilimufanyia Yawe kiapo nikisema kama Yawe akinirudisha Yerusalema basi, nitamwabudu yeye.”


Kisha, mufalme akamwambia Simei: “Wewe hautauawa.” Mufalme akamwapia Simei.


Mufalme akamwambia: “Usiniambie zaidi juu ya mambo yako pekee. Mimi nimekwisha amua kuwa wewe pamoja na Siba mutagawanyana inchi ya Saulo.”


Namani akasema: “Ikiwa hautapokea zawadi zangu, basi tafazali umupatie mutumishi wako udongo unaoweza kubebwa na nyumbu wawili, maana tokea leo mimi mutumishi wako sitatoa sadaka za kuteketezwa wala sadaka kwa miungu mingine lakini tu kwa Yawe.


Lakini Yebesi alimwomba Mungu wa Israeli akisema: “Ee Mungu, ninakusihi unibariki na kupanua mipaka yangu. Mukono wako ukuwe pamoja nami na unilinde kutokana na jambo lolote ovu, na mateso yasinipate.” Naye Mungu akamupa yale aliyoomba.


Yawe ananijalia nguvu na uwezo, yeye mwenyewe ndiye anayeniokoa. Yeye ni Mungu wangu nami nitamusifu; ni Mungu wa baba yangu nami nitamutukuza.


Leo Yawe ameahidi kwamba atakuwa Mungu wenu, kama mutafuata njia zake na kushika masharti, amri, na maagizo yake na kutii sauti yake.


basi, yeyote atakayetoka inje kutoka katika nyumba yangu kuja kunipokea nitakapokuwa ninarudi nyuma ya kuwashinda Waamoni, huyo atakuwa wako wewe Yawe. Nitakutolea kama sadaka ya kuteketezwa.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ