Mwanzo 28:18 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
18 Yakobo akaamuka asubui mapema, akatwaa lile jiwe alilokuwa ameliweka chini ya kichwa chake, akalisimika kama nguzo na kulitakasa kwa kulimiminia mafuta.
Hivyo, asubui mapema, Abrahamu akatwaa chakula na chupa la maji, akamupa Hagari na kumubebesha mutoto juu ya bega. Akamufukuza pamoja na mwana wake. Hagari akaondoka, akakuwa anatangatanga katika jangwa la Beri-Seba.
Basi, kesho yake, Abrahamu akaamuka asubui mapema, akatandika punda wake, akawatwaa watumishi wake wawili pamoja na Isaka mwana wake. Akatayarisha kuni kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa kwa moto, kisha akaanza safari kuelekea pahali alipoambiwa na Mungu.
Mimi ndimi yule Mungu aliyekutokea kule Beteli, pahali pale ulipotakasa lile jiwe kwa kulimiminia mafuta na ambapo ulifanyia kiapo. Sasa ondoka katika inchi hii urudi katika inchi yako.’ ”
Abusaloma, alipokuwa angali anaishi, alikuwa amejijengea na kujisimikia nguzo inayokuwa kwenye Bonde la Mufalme, maana alisema: “Mimi sina mutoto mwanaume wa kudumisha jina langu kusudi nikumbukwe.” Nguzo hiyo aliipa jina lake, na inaitwa “Nguzo ya Abusaloma” mpaka leo.
Siku Musa alipomaliza kusimamisha hema takatifu, akalimiminia mafuta na kulitakasa pamoja na vyombo vyake vyote. Akamiminia mazabahu mafuta na kuitakasa pamoja na vyombo vyake vyote.
Yoshua akasimika vilevile mawe kumi na mawili katikati ya muto Yordani, pahali pale miguu ya makuhani waliobeba lile Sanduku la Agano iliposimama. Mawe hayo yako kule mpaka hivi leo.