Tera akatwaa Abramu mwana wake, Loti mujukuu wake aliyekuwa mwana wa Harani, na Sarai muke wa Abramu, wakaondoka wote pamoja toka Uri, muji wa Wakaldea, na kwenda katika inchi ya Kanana. Lakini walipofika Harani, wakakaa pale.
Kwa hiyo, Abramu akaondoka kama vile Yawe alivyomwamuru, na Loti akakwenda pamoja naye. Abramu alikuwa na umri wa miaka makumi saba na mitano alipotoka Harani.
Alitwaa Sarai muke wake, na Loti mwana wa ndugu yake, pamoja na mali yao yote na watu wote waliokuwa wamejipatia kule Harani, wakaondoka kuelekea inchi ya Kanana. Walipoingia katika inchi ya Kanana,
Kisha Yakobo akamwomba Mungu akisema: “Ee Mungu wa babu yangu Abrahamu, Mungu wa baba yangu Isaka! Ewe Yawe uliyeniambia nirudi katika inchi yangu kwa jamaa yangu, ukaniahidi kunitendea mema,
Siku moja, Mungu akamwambia Yakobo: “Anza safari, uende kuishi Beteli na kunijengea mazabahu kule, mimi Mungu niliyekutokea wakati ulipomukimbia kaka yako Esau.”
Akajenga mazabahu pahali pale na kupaita “Mungu wa Beteli” maana ni pale ndipo pahali Mungu alipojionyesha kwake wakati alipokuwa akimukimbia kaka yake.
Yawe akamwambia Musa: Anza safari uondoke hapa, wewe na watu hao uliowatoa katika inchi ya Misri. Muende katika inchi niliyowapia Abrahamu, Isaka na Yakobo, nikisema: Nitawapa wazao wenu inchi hii.
Watu wa Gileadi walikuwa waovu sana; hakuna tena kitu kinachokuwa chao. Kule Gilgali walitambikia ngombe dume. Hivyo, mazabahu zao zitakuwa malundo ya mawe yaliyowekwa kwa mafungu katika shamba.
Stefano akamujibu: “Wandugu zangu na wababa zangu, munisikilize! Mungu mwenye utukufu alimutokea babu yetu mukubwa Abrahamu wakati alipokuwa angali katika inchi ya Mesopotamia, mbele hajahamia katika muji Harani.