Yawe akamwambia: “Mataifa mawili yako ndani ya tumbo lako; makabila mawili yatakayozaliwa nawe, yatatengana. Moja litakuwa lenye nguvu kuliko lingine, mukubwa atamutumikia mudogo.”
Jamii za watu zikutumikie, na mataifa yainame mbele yako kwa heshima. Ukuwe mutawala wa wandugu zako, na wana wa mama yako wainame mbele yako kwa heshima. Kila mutu anayekulaani alaaniwe, kila mutu anayekubariki abarikiwe!”
Sasa, wewe Amazia umewashinda kabisa Waedomu, na moyo wako unakufanya ujivune. Ufurahie utukufu wako, ukae katika nyumba yako; kwa nini kujitafutia taabu zitakazokuangamiza wewe mwenyewe pamoja na watu wako wa Yuda?”
Hivyo Waedomu wakaasi utawala wa Yuda mpaka sasa. Wakati uleule, vilevile wakaaji wa Libuna nao wakaasi utawala wake kwa sababu Yoramu alikuwa amemwacha Yawe, Mungu wa babu zake.