Esau akasema: “Ndiyo maana anaitwa Yakobo! Ametwaa nafasi yangu mara mbili. Kwanza alitwaa haki yangu ya muzaliwa wa kwanza, na sasa ametwaa baraka yangu.” Kisha akamwuliza baba yake: “Basi, haukuniwekea baraka yoyote?”
Kama munavyojua, nyuma ya pale alikataliwa wakati alipotaka kupokea baraka toka kwa baba yake. Yeye hakukuwa tena na namna ya kugeuza tendo lake ijapokuwa alitafuta baraka ile kwa machozi.