Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 27:29 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

29 Jamii za watu zikutumikie, na mataifa yainame mbele yako kwa heshima. Ukuwe mutawala wa wandugu zako, na wana wa mama yako wainame mbele yako kwa heshima. Kila mutu anayekulaani alaaniwe, kila mutu anayekubariki abarikiwe!”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 27:29
40 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Anayekubariki, nitamubariki, anayekulaani, nitamulaani. Kwa njia yako, nitabariki mataifa yote ya dunia.”


Yakobo akamwambia: “Uniapie kwanza.” Basi, Esau akamwapia na kumwuzishia Yakobo haki yake ya muzaliwa wa kwanza.


Isaka alipokwisha kumubariki Yakobo, naye Yakobo alipokuwa angali tu anatoka mbele ya baba yake Isaka, Esau kaka ya Yakobo, akarudi kutoka katika mawindo.


Isaka akamujibu: “Nimekwisha kumufanya Yakobo kuwa mutawala wako, na kumupa wandugu zake wote kuwa watumishi wake. Nimemupatia ngano na divai. Nikufanyie nini sasa, wewe mwana wangu?”


Utaishi kwa upanga wako, na utamutumikia ndugu yako; lakini utakapoasi utaivunja nira yake toka kwenye shingo yako.”


Lakini alipomwelezea baba yake na wandugu zake ndoto hiyo, baba yake alimukaripia, akisema: “Ni ndoto gani hiyo uliyoota? Itatupasa mimi, mama yako na wandugu zako kuja kuinama chini kwa heshima mbele yako?”


Niliota kwamba sisi wote tulikuwa katika shamba tukifunga miganda. Kwa rafla muganda wangu ukainuka na kusimama wima. Miganda yenu ikakusanyika kuuzunguka na kuinamia mbele ya muganda wangu.”


Mungu amuzidishe Yafeti, aishi katika hema za Semu; Kanana akuwe mutumwa wake.”


Waasherati wote wa kidini waliobaki tangu nyakati za baba yake Asa, Yosafati aliwaondoa katika inchi.


Ingawa kabila la Yuda ndilo lililokuja kuwa lenye nguvu zaidi kuliko mengine, na watawala walitoka mule, haki ya muzaliwa wa kwanza ilikuwa ya Yosefu).


Atawale kutoka bahari hata bahari, kutoka muto Furati hata miisho ya dunia.


Yawe anasema hivi: Utajiri wa Misri na faida ya uchuuzi za Kushi, pamoja na za watu wa Seba, wale watu warefu sana, zitakuja kwako mwenyewe wewe taifa la Israeli, zote zitakuwa mali yako. Watu hao watakufuata wakifungwa minyororo; watainama mbele yako na kukusihi wakisema: Kwako kuna Mungu wa kweli, wala hakuna Mungu mwingine lakini yeye.


Wafalme watakushugulikia, na malkia watakutengenezea chakula. Watainama mbele yako uso mpaka chini, na kulambula mavumbi ya miguu yako. Halafu utatambua kwamba mimi ni Yawe; wote wanaonitegemea hawatapata haya.


Yawe, Mukombozi na Mutakatifu wa Israeli, anamwambia hivi yule anayezarauliwa sana, yule anayechukiwa na mataifa, na ambaye ni mutumishi wa watawala: Wafalme wataona nao watasimama; wakubwa watainama na kuabudu kwa heshima ya Yawe ambaye anatimiza ahadi zake, kwa heshima ya Mutakatifu wa Israeli ambaye amekuchagua wewe.


Kila ufalme au taifa lisilokutumikia litaangamizwa; mataifa hayo yatateketezwa kabisa.


Wazao wa wale waliokutesa, watakuja na kuinama uso mpaka chini mbele yako. Wote wale waliokuzarau, watapiga magoti kwenye miguu yako. Watakuita: “Muji wa Yawe”, “Sayuni”, “Muji wa Mutakatifu wa Israeli”.


Yawe ametoa neno juu ya Yakobo nalo litamupata Israeli.


Nitamulaani namna gani mutu ambaye Mungu hakumulaani? Nitawakaripia watu ambao Yawe hakuwakaripia?


Edomu itakuwa urizi wake, Seiri itakuwa mali yake, Israeli itapata ushindi mukubwa.


Atavizia na kulala chini kama simba, nani atasubutu kumwamusha? Abarikiwe yeyote atakayekubariki wewe Israeli, alaaniwe yeyote atakayekulaani.


Mufalme atawajibu: ‘Kweli ninawaambia: kila kitu mulichokitendea mumoja wa hawa wandugu zangu wanaohesabiwa kuwa wadogo, mulinitendea mimi.’


Naye mufalme atawajibu: ‘Kweli ninawaambia: kila kitu mulichokosa kumutendea mumoja wa hawa wanaohesabiwa kuwa wadogo, hamukunitendea mimi.’


Na juu ya nguo yake na paja la muguu wake kulikuwa kumeandikwa jina hili: “Mufalme wa wafalme na Bwana wa wabwana.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ