Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 27:27 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

27 Basi, Yakobo akamukaribia baba yake na kumubusu, na baba yake aliposikia harufu ya nguo zake, akamubariki akisema: “Hii ni harufu nzuri ya mwana wangu. Ni kama harufu ya shamba Yawe alilobariki!

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 27:27
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mwaka ule Isaka akapanda mbegu katika inchi ile, akavuna mara mia zaidi, maana Yawe alimubariki,


Kisha Rebeka akatwaa nguo bora za Esau, mwana wake mukubwa, alizokuwa nazo kwa nyumba, akamuvalisha Yakobo, mwana wake mudogo.


Halafu baba yake Isaka, akamwambia: “Sogea karibu, mwana wangu, unibusu.”


Kwa hiyo Isaka, baba yake, akamwambia: “Makao yako yatakuwa mbali na udongo wenye mboleo, na mbali na umande wa mbinguni.


Macho ya Israeli yalikuwa hayaoni vizuri kwa sababu ya uzee. Basi, Yosefu akasogeza wana wake karibu na baba yake, naye akawabusu na kuwakumbatia.


Kisha Israeli akamubariki Yosefu, akisema: “Mungu ambaye babu zangu Abrahamu na Isaka walimutii katika maisha yao, Mungu ambaye ameniongoza katika maisha yangu mpaka leo,


Wewe unatunza udongo kwa kuunyeshea mvua, unaujalia mboleo na kuustawisha; muto wako umejaa maji tele, unaifanikisha inchi na kuipatia mavuno. Hivi ndivyo unavyotayarisha udongo.


Miti ya tini imeanza kuzaa na mizabibu imechanua. Inatoa harufu nzuri. Kuja, basi, ewe mupenzi wangu unayenipendeza, kuja tuende.


Juu ya kabila la Yosefu akasema: “Yawe abariki inchi yake, kwa baraka nzuri kabisa kutoka juu,


Kwa njia ya imani, Isaka aliwabariki Yakobo na Esau kuelekea mambo ya siku zitakazokuja.


Udongo unaonyeshewa na mvua mara kwa mara na kutoa mimea inayofaa kwa walimaji, unabarikiwa na Mungu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ