Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 27:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

19 Yakobo akamujibu baba yake: “Ni mimi Esau, muzaliwa wako wa kwanza. Nimefanya kama ulivyoniagiza. Tafazali baba, amuka uikae ukule nyama ya mawindo yangu kusudi upate kunibariki.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 27:19
15 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wa kwanza alikuwa mwekundu, mwenye nywele mwili wote; hivyo wakamwita Esau.


Basi, Isaka akamupenda Esau kwa sababu alipenda kula nyama wa mawindo yake, lakini Rebeka akamupenda Yakobo.


Basi, Yakobo akaingia ndani kwa baba yake, akamwita: “Baba!” Naye akaitika: “Niko hapa! Ni nani wewe mwana wangu?”


Halafu Isaka akamwambia Yakobo: “Basi, mwana wangu, karibia nipate kukupapasa kusudi nijue kweli kama wewe ndiwe mwana wangu Esau au hapana.”


Esau vilevile akatengeneza chakula kitamu, akamupelekea baba yake, akamwambia: “Basi baba, amuka ukule nyama ya mawindo yangu mimi mwana wako, upate kunibariki!”


Lakini Isaka akasema: “Ndugu yako alikuja kwa udanganyifu, naye ametwaa baraka yako.”


Halafu unitengenezee chakula kitamu, kile ninachopenda, uniletee nikule, nipate kukubariki mbele ya kufa kwangu.”


Kasirani yake itakapopoa juu yako, naye atakapokuwa amesahau mambo uliyomutendea, nitatuma mutu kwa kukutafuta kule. Kwa nini nikufiwe na ninyi wote wawili siku moja?”


Yule muzee wa Beteli akamwambia: “Mimi vilevile ni nabii kama wewe, na Yawe amesema nami kwa njia ya malaika akisema: ‘Umurudishe kwako, akule chakula na kunywa maji.’ ” Lakini yule nabii muzee alikuwa anamudanganya tu.


Yeroboamu akamwambia muke wake: “Ujigeuze kusudi watu wasitambue kwamba wewe ni muke wangu, uende Shilo kwa nabii Ahiya aliyesema kwamba mimi nitakuwa mufalme wa Israeli.


Ninyi munajidai mumefanya agano na kifo mumefanya mapatano na kuzimu! Ninyi munasema kwamba hasara itakapokuja haitawapata, kwa sababu mumefanya uongo kuwa tegemeo lenu, na udanganyifu kuwa kikingio chenu!


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ