32 Siku ileile watumishi wa Isaka walimufikia na kumupasha habari za kile kisima walichokuwa wamechimba, wakasema: “Tumepata maji!”
Kwa hiyo, Isaka akajenga mazabahu kule na kumwabudu Yawe. Akapiga kambi kule, na watumishi wake wakachimba kisima.
Kesho yake wakaamuka asubui mapema na kufanya kiapo. Kisha Isaka akawasindikiza na kuagana nao kwa amani.
Basi, Isaka akakiita kisima hicho Siba, ni kusema “Kiapo”. Kwa hiyo jina la muji ule ni Beri-Seba hata leo.
Uvivu unasababisha umasikini, lakini mukono wa mutu wa bidii unajitajirisha.
Muvivu anatamani lakini hapati kitu chochote, wakati mwenye bidii anajaliwa kwa wingi.
“Muombe, nanyi mutapewa; mutafute, nanyi mutapata; mupige hodi, nanyi mutafunguliwa mulango.