Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 26:28 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

28 Wao wakamujibu: “Tumeona wazi kwamba Yawe yuko pamoja nawe. Kwa hiyo, tunafikiri inafaa tufanye kiapo pamoja nawe na kufanya agano,

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 26:28
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

nami nitakuapisha kwa jina la Yawe, Mungu wa mbingu na dunia, kwamba hautamwoea mwana wangu binti yeyote kati ya wabinti za Wakanana ninaoishi nao.


Utakapofika kwa jamaa yangu, nao wasipokupa yule binti, basi, hautafungwa na kiapo changu.’


Basi, tufanye agano mimi nawe, likuwe ushuhuda kati yako nami.”


Yule bwana wake akatambua kwamba Yawe alikuwa pamoja na Yosefu, na kwamba ndiye aliyefanikisha mambo yote Yosefu aliyofanya.


Tokea wakati Potifari alipomufanya Yosefu kuwa musimamizi wa nyumba yake na mwangalizi wa mali yake, Yawe akabariki nyumba ya yule Mumisri kwa ajili ya Yosefu. Baraka za Yawe zikakuwa juu ya kila kitu alichokuwa nacho, ndani ya nyumba na katika shamba.


Solomono, mwana wa mufalme Daudi, alijiimarisha katika utawala wake, naye Yawe, Mungu wake akamubariki na kumufanya akuwe mukubwa sana.


Asa akakusanya watu wote wa Yuda na Benjamina, na wengine wote waliokuwa wakikaa katika inchi yake kutoka kabila la Efuraimu, la Manase na la Simeoni. Hawa walikuja kwake walipoona kwamba Yawe, Mungu wake yuko pamoja naye.


Yawe anasema hivi: Utajiri wa Misri na faida ya uchuuzi za Kushi, pamoja na za watu wa Seba, wale watu warefu sana, zitakuja kwako mwenyewe wewe taifa la Israeli, zote zitakuwa mali yako. Watu hao watakufuata wakifungwa minyororo; watainama mbele yako na kukusihi wakisema: Kwako kuna Mungu wa kweli, wala hakuna Mungu mwingine lakini yeye.


Wazao wa wale waliokutesa, watakuja na kuinama uso mpaka chini mbele yako. Wote wale waliokuzarau, watapiga magoti kwenye miguu yako. Watakuita: “Muji wa Yawe”, “Sayuni”, “Muji wa Mutakatifu wa Israeli”.


Nanyi mutaitwa: “Makuhani wa Yawe”, Mutaitwa: “Watumishi wa Mungu wetu”. Mutafaidika kwa utajiri wa mataifa, mutatukuzwa kwa mali zao.


Wazao wao watajulikana kati ya mataifa; watajulikana kati ya watu wengine. Kila mutu atakayewaona atakubali kwamba wao ni watu waliobarikiwa na Yawe.


Basi kufuatana na mambo hayo, tuseme nini zaidi? Mungu akiwa upande wetu, ni nani anayeweza kupingana nasi?


kufichuliwa waziwazi mawazo yake aliyoficha. Na hivi atainama uso mpaka chini na kumwabudu Mungu, akisema: “Kweli Mungu ni katikati yenu!”


Musijiachilie kutawaliwa na tamaa ya mali katika maisha yenu, lakini mutoshelewe na vitu munavyokuwa navyo, kwa maana Mungu mwenyewe amesema: “Sitakusahau wala kukuachilia.”


Kwa maana watu wanapofanya kiapo, wanaapa kwa jina la mutu anayekuwa mukubwa kuliko wao wenyewe, nao uhakikisho wa kiapo kile unakomesha mabishano yote kati yao.


Yawe akamwambia Yoshua: “Leo hii, nitaanza kukutukuza mbele ya watu wote wa Israeli kusudi wajue kwamba, kama vile nilivyokuwa pamoja na Musa, ndivyo vilevile nitakavyokuwa pamoja nawe.


Mufalme Nahasi wa Waamoni, alikwenda na kuushambulia muji wa Yabesi-Gileadi. Wakaaji wa muji wa Yabesi-Gileadi wakamwambia Nahasi: “Fanya mapatano nasi, nasi tutakutumikia.”


Lakini Saulo alipoona wazi kwamba Yawe alikuwa pamoja na Daudi, na kwamba Mikali binti yake alimupenda sana Daudi,


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ