Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 26:27 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

27 Isaka akawauliza: “Kwa nini mumekuja kwangu ijapokuwa munanichukia na mulinifukuza kwenu?”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 26:27
9 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Alikuwa na makundi ya kondoo, ngombe na watumwa wengi. Kwa hiyo, Wafilistini wakamwonea wivu.


Halafu Abimeleki akamwambia Isaka: “Ondoka kwetu, maana wewe umetuzidi nguvu.”


Wao wakamujibu: “Tumeona wazi kwamba Yawe yuko pamoja nawe. Kwa hiyo, tunafikiri inafaa tufanye kiapo pamoja nawe na kufanya agano,


Kisha Yosefu akatuma wajumbe kwenda kumwita baba yake Yakobo pamoja na jamaa yake yote wafike Misri. Nao wote kwa jumla walikuwa makumi saba na tano.


Lakini yule aliyekuwa akimutendea mwenzake vibaya akamusukuma Musa pembeni akisema: ‘Nani aliyekuweka wewe kuwa mukubwa na mwamuzi wetu?


“Huyu Musa ndiye yule Waisraeli waliyemukataa, wakisema: ‘Nani aliyekuweka wewe kuwa mukubwa na mwamuzi?’ Mungu alimutuma kuwa mukubwa na mukombozi wao, akisaidiwa na yule malaika aliyemutokea katikati ya kichaka kinachowaka moto.


“Wale babu wakamwonea Yosefu wivu hata wakamwuzisha kuwa mutumwa katika inchi ya Misri. Lakini Mungu akamulinda,


Angalia, nitakupa watu wa kikundi chenye kuabudu Shetani, ndio wale wasema uongo wanaojidai kwamba wao ni Wayuda, lakini ni wadanganyifu. Hakika nitawalazimisha kupiga magoti mbele yako, nao watajua ya kuwa mimi ninakupenda.


Lakini Yefuta akawaambia hao wazee wa Gileadi: “Si mulinichukia hata mukanifukuza kutoka kwa jamaa ya baba yangu? Kwa nini munanifikia sasa mukiwa katika taabu?”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ