21 Halafu wakachimba kisima kingine, nacho vilevile wakakigombania; hivyo Isaka akakiita kisima hicho “Fitina”.
Wakati ule Abrahamu alikuwa amemwonya Abimeleki juu ya kisima cha maji ambacho watumishi wa Abimeleki walikuwa wamemunyanganya.
wachungaji wa pale Gerari wakagombana na wachungaji wa Isaka wakisema: “Maji haya ni yetu.” Hivyo Isaka akakiita kisima hicho “Ugomvi” kwa sababu waligombana naye.
Kisha Isaka akakwenda pahali pengine na kuchimba kisima kingine. Lakini hicho hawakukigombania. Hivyo Isaka akakiita “Nafasi Pana”, akisema: “Sasa Yawe ametuachia nafasi, nasi tutastawi katika inchi hii.”
Kwa mwanzo wa utawala wa mufalme Ahasuero, waadui za watu waliokaa Yuda na Yerusalema wakaandika mashitaki juu yao.