Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 26:18 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

18 Isaka akachimba vile visima vilivyokuwa vimechimbwa wakati Abrahamu baba yake alipokuwa muzima, visima ambavyo Wafilistini walikuwa wameziba nyuma ya kifo cha Abrahamu. Akavipa majina yaleyale baba yake aliyovipa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 26:18
10 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wakati ule Abrahamu alikuwa amemwonya Abimeleki juu ya kisima cha maji ambacho watumishi wa Abimeleki walikuwa wamemunyanganya.


Abrahamu akamujibu: “Hawa wana-kondoo dike saba ninakupa kwa mukono wangu mwenyewe kama ushuhuda wangu kwamba mimi ndiye niliyechimba kisima hiki.”


Kwa hiyo kisima hicho kikaitwa Beri-Seba, maana wote wawili walifanya kiapo pahali pale.


Basi, Isaka akaondoka kule, akapiga kambi yake katika bonde la Gerari, akakaa kule.


Lakini watumishi wa Isaka walipochimba katika lile bonde na kupata kisima cha maji yanayobubujika,


Hata katika jangwa vilevile alijenga minara, akachimba visima vingi, maana alikuwa na makundi mengi ya nyama kwenye sehemu za miinuko na mabonde. Alikuwa na walimaji na watunza mizabibu kwenye milima, na katika inchi yenye mboleo maana alipenda mulimo.


Lakini wanaoabudu miungu mingine, watapata mateso mengi. Sitaitolea sadaka za damu hata kidogo, na majina ya miungu hiyo sitayataja.


Huko nitamurudishia mashamba yake ya mizabibu. Bonde la Akori litakuwa mulango wa tumaini. Ataniitikia vizuri kama vile alipokuwa kijana, kama wakati alipotoka katika inchi ya Misri.


Wakati ule, nitaondoa majina ya sanamu za miungu katika inchi, wala hayatakumbukwa tena. –Ni ujumbe wa Yawe wa majeshi.– Na wanaojidai kuwa manabii nitawaondoa kabisa pamoja na tamaa zao za kuabudu sanamu.


Nebo na Bali-Meoni (majina ya hiyo miji yalibadilishwa), na Sibuma. Miji waliyoijenga wakaipa majina mengine.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ