Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 26:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Mwaka ule Isaka akapanda mbegu katika inchi ile, akavuna mara mia zaidi, maana Yawe alimubariki,

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 26:12
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Sasa Abrahamu alikuwa muzee wa miaka mingi, naye Yawe alikuwa amemubariki katika kila hali.


Yawe amemubariki sana bwana wangu, naye amekuwa mutu mukubwa. Amemupa makundi ya kondoo na nyama wengi, feza na zahabu, watumishi wanaume na wanawake, ngamia na punda!


Nyuma ya kifo cha Abrahamu, Mungu alimubariki mwana wake Isaka. Naye Isaka akaishi karibu na kisima cha Beri-Lahai-Roi.


kwamba hautatuzuru, nasi vilevile hatutakuzuru. Tulikutendea tu vizuri, tukakuacha uende kwa amani, bila kukutendea ubaya wowote. Na sasa wewe ni mubarikiwa wa Yawe.”


Ukae katika inchi hiyo, nami nitakuwa pamoja nawe na kukubariki. Nitatimiza ahadi niliyomupa baba yako Abrahamu, maana nitakupa wewe na wazao wako inchi hizi zote.


Mbele sijakuja ulikuwa na mali chache tu lakini tangu nifike, mali yako imeongezeka kwa wingi sana, na Yawe amekubariki kila fasi nilikokwenda. Lakini sasa, nitatunza wakati gani jamaa yangu mwenyewe?”


Katika miaka ya Yobu iliyofuata, Yawe alimubariki zaidi kuliko hata alivyokuwa amemubariki pale mbele. Basi Yobu akakuwa na kondoo elfu kumi na ine, ngamia elfu sita, ngombe elfu mbili na punda dike elfu moja.


Watu wakusifu, ee Mungu, watu wote wakusifu!


Inchi itoe mazao kwa wingi, vilima vijae mavuno kama ya Lebanoni, na watu wa miji wastawi kama majani.


Baraka za Yawe ndizo zinazoleta utajiri. Juhudi za mutu haziongezi kitu.


Panda mbegu asubui na usiache kupanda mpaka magaribi, maana, haujui mbegu gani zitaota; za asubui, za magaribi, au zote zitakuwa nzuri.


Sasa nitaleta tena amani katika dunia, mvua itanyesha kama kawaida, udongo utatoa mazao, na mizabibu itazaa kwa wingi. Nitawapa watu wanaobaki wa taifa hili yale yote yakuwe mali yao.


Pahali zile mbegu zilipoanguka katika udongo muzuri ni mufano wa watu wanaosikia Neno la Mungu na kulielewa. Nao wanazaa matunda; wamoja matunda mia moja, wengine makumi sita na wengine makumi tatu.”


Lakini mbegu zingine zikaanguka katika udongo muzuri na kutoa matunda: zimoja zikazaa punje mia moja, zingine makumi sita na zingine makumi tatu.


Lakini mbegu zingine zikaanguka katika udongo muzuri, mimea ikaota, ikakomaa na kuzaa matunda: zimoja zikazaa punje makumi tatu, zingine makumi sita na zingine punje mia moja.”


Mimi nilipanda mbegu na Apolo alinyweshea maji, lakini Mungu ndiye aliyeiotesha.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ