Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 26:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Kisha kukatokea njaa katika inchi ile, nyuma ya ile ya kwanza iliyokuwa kwa wakati wa Abrahamu. Isaka akakwenda Gerari kwa Abimeleki mufalme wa Wafilistini.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 26:1
10 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wakati ule, njaa ikatokea katika inchi. Njaa hiyo ilikuwa kali, hivyo Abramu akalazimika kwenda Misri kukaa kule kwa muda.


Nyuma ya kifo cha Abrahamu, Mungu alimubariki mwana wake Isaka. Naye Isaka akaishi karibu na kisima cha Beri-Lahai-Roi.


Halafu Yakobo akamupa Esau mukate na muchuzi wa manjegere. Esau akakula, akakunywa, kisha akaondoka, akajiendea. Hivi ndivyo Esau alivyoizarau haki yake ya muzaliwa wa kwanza.


Basi, wana wa Israeli wakafika Misri wakiwa kati ya wanunuzi wengine, maana hata katika inchi ya Kanana kulikuwa njaa.


Kisha njaa ikazidi kuwa kali katika inchi ya Kanana.


Wakati mumoja katika siku za utawala wa Daudi kukatokea njaa kali katika inchi. Njaa hiyo ilidumu miaka mitatu yenye kufuatana. Daudi alimwomba Yawe shauri. Yawe akamwambia: “Saulo na jamaa yake wana makosa ya kumwanga damu kwa sababu aliwaua Wagibeoni.”


Yawe akamwambia Musa: Anza safari uondoke hapa, wewe na watu hao uliowatoa katika inchi ya Misri. Muende katika inchi niliyowapia Abrahamu, Isaka na Yakobo, nikisema: Nitawapa wazao wenu inchi hii.


Hapo zamani, wakati waamuzi walipokuwa wanatawala Waisraeli, kulitokea njaa katika inchi. Mutu mumoja kutoka Betelehemu katika Yuda pamoja na muke wake na watoto wao wanaume wawili walikwenda kuishi kwa muda katika inchi ya Moabu kwa kuishi kama wageni.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ