Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 25:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Abrahamu akamurizisha Isaka mali yake yote.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 25:5
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yawe amemubariki sana bwana wangu, naye amekuwa mutu mukubwa. Amemupa makundi ya kondoo na nyama wengi, feza na zahabu, watumishi wanaume na wanawake, ngamia na punda!


Sara, muke wa bwana wangu katika uzee wake, alimuzalia bwana wangu mutoto; na bwana wangu amemupa yule mutoto mali yake yote.


Wana wa Midiani walikuwa Efa, Eferi, Hanoki, Abida na Elda. Wote hao walikuwa wazao wa Ketura.


Alikuwa na makundi ya kondoo, ngombe na watumwa wengi. Kwa hiyo, Wafilistini wakamwonea wivu.


Bwana anakuja kwenye pahali pake patakatifu kutoka Sinai, akikuwa na kundi kubwa, na maelfu na maelfu ya magari ya kukokotwa.


“Baba yangu ameweka vitu vyote katika mikono yangu. Hakuna mutu anayemujua Mwana isipokuwa Baba, wala hakuna anayemujua Baba isipokuwa Mwana, na yeyote Mwana anayetaka kumujulisha kwake.


Kisha Yesu akakuja karibu nao, na kuwaambia: “Nimepewa mamlaka yote mbinguni na katika dunia.


Kwa maana ulimupa mamlaka juu ya watu wote, kusudi awapatie uzima wa milele wale wote uliomupa.


Baba anamupenda Mwana wake, naye ameweka vitu vyote kwa mukono wake.


Na kama sisi ni watoto, basi tutakuwa na sehemu katika urizi ule Mungu aliowaahidi watu wake, na tutashiriki pamoja na Kristo katika urizi ule; kwa maana kama tukiteswa pamoja naye tutatukuzwa pamoja naye vilevile.


Yeye hakumwacha Mwana wake wa pekee, lakini alimutoa kwa ajili yetu sisi wote. Namna gani atakosa kutupatia vilevile vitu vyote kwa njia ya mwana wake?


Kama ninyi ni watu wa Kristo, basi, ninyi ni wazao wa Abrahamu, ninyi mutakuwa warizi sawa vile Mungu alivyoahidi.


Nanyi wandugu ni watoto wa Mungu waliozaliwa kutokana na ahadi yake kama vile Isaka.


Kwa maana Mungu mwenyewe alitaka ukamilifu wake uonekane ndani ya mwana wake.


Lakini kwa siku hizi za mwisho amesema nasi kwa njia ya Mwana wake. Mungu alimuweka kuwa murizi wa vitu vyote, na ambaye kwa njia yake aliumba ulimwengu wote.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ