Makundi ya ngamia yataifunika inchi yako, wana wa ngamia kutoka Midiani na Efa; wote watakuja kutoka Seba. Watakuletea zahabu na ubani, wakitangaza sifa za Yawe.
Mukimbie, enyi wakaaji wa Dedani, mugeuke na kujificha ndani ya mapango! Maana nitawaletea maangamizi, enyi wazao wa Esau; wakati wa kuwaazibu umefika.
basi, Bwana wetu Yawe anasema: Nitanyoosha mukono juu ya inchi ya Edomu kwa kuwaazibu na kuwaua watu wote na nyama. Nitaifanya kuwa ukiwa kutoka muji wa Temani mpaka muji wa Dedani. Watu wa inchi hiyo watauawa kwa upanga.
Watu wa Dedani walifanya biashara nawe. Inchi nyingi za kandokando ya bahari zilikuwa masoko yako makubwa. Watu wake walikuletea pembe za tembo na miti mizuri inayoitwa ebene kwa kununua vitu kwako.
Walitwaa miti ya mialo toka Basani wakakuchongea makasia; walikutengenezea mbao za kuikalia kwa miti ya misunobari ya kisanga cha Kipuro, na kuipamba kwa pembe ya tembo.