“Na juu ya Isimaeli, nimesikia ombi lako. Nitamubariki, nitamujalia watoto wengi na kuwazidisha sana. Isimaeli atakuwa baba wa watawala kumi na wawili, nami nitamufanya kuwa baba wa taifa kubwa.
Kisha Abrahamu akamutahiri mwana wake Isimaeli, na kuwatahiri watumwa wanaume wote waliozaliwa katika nyumba yake na walionunuliwa kwa feza zake. Aliwatahiri wote siku hiyohiyo kama vile Mungu alivyomwamuru.