Mungu akawabariki na kuwaambia: “Muzae, muongezeke, na mujaze inchi na kuitawala. Mutawale samaki wa bahari, ndege wa anga, na kila kiumbe chenye uzima kinachotembea katika dunia.”
Kutoka kiti hicho kijito cha moto kilibubujika, kikatiririka. Maelfu ya watu walimutumikia, na mamilioni walisimama mbele yake. Halafu waamuzi wakajitayarisha kwa kuhukumu, na vitabu vikafunguliwa.
Hao watumwa unaweza kuwapatia watoto wako wakuwe mali yao milele. Hao unaweza kuwafanya watumwa wako, lakini kuelekea ndugu yako Mwisraeli, usimutawale kwa kinguvu.