6 Abrahamu akamwambia: “Hapana! Angalia sana usimurudishe mwana wangu kule.
Mutumishi akamwambia: “Labda mwanamuke yule atakataa kunifuata kuja huku, ikiwa hivyo, ni lazima nimurudishe mwana wako katika inchi ulikotoka?”
Ikiwa mwanamuke yule hatapenda kukufuata mpaka huku, basi kiapo changu hakitakufunga, lakini kwa vyovyote vile usimurudishe mwana wangu kule.”
Kristo ametukomboa katika utumwa kusudi tukuwe huru kabisa. Basi, musimame imara wala musijitie tena katika vifungo vya utumwa.
Lakini sisi si watu wenye kurudi nyuma na kupotea, lakini sisi ni watu wenye imani na wenye kuokoka.
Kwa njia ya imani, aliishi kama vile mugeni katika inchi ile Mungu aliyomwahidi. Yeye alikuwa akiishi katika hema kama vile Isaka na Yakobo walivyoishi. Wao vilevile walishiriki pamoja naye ahadi ile ile ya Mungu.