Kisha, yule mutumishi akatwaa ngamia kumi wa bwana wake akaondoka akiwa na zawadi nzuri za kila aina. Akasafiri kwenda katika muji Nahori alimokaa, katika inchi ya Mesopotamia.
Ngamia walipotosheka kunywa maji, yule mutu akamupa yule binti pete ya zahabu yenye uzito wa yapata grama sita, na vikomo viwili vya zahabu za grama kumi kila moja.
Baba yao aliwapa zawadi kubwakubwa za feza, zahabu na vitu vingine vya bei kali, na vilevile miji ya Yuda yenye kuta. Lakini kwa sababu Yoramu ndiye aliyekuwa muzaliwa wake wa kwanza, Yosafati akamupa ufalme atawale kwa pahali pake.
Kila mwanamuke Mwebrania atamwomba jirani yake Mumisri, au mugeni wake anayekuwa katika nyumba yake, amupe vyombo vya feza na zahabu pamoja na nguo. Hivyo mutawavalisha watoto wenu wanaume na wanawake. Ndivyo mutakavyowanyanganya Wamisri mali yao.”
Basi, Hezekia aliwakaribisha na kuwaonyesha nyumba alimoweka mali yake: feza, zahabu, viungo vya kukoleza chakula, mafuta ya bei kali, vifaa vyake vyote vya vita na vitu vyote vilivyokuwa katika gala zake. Hakuna chochote katika nyumba yake ya kifalme au katika inchi yake ambacho hakuwaonyesha.