Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 24:27 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

27 akisema: “Atukuzwe Yawe, Mungu wa bwana wangu Abrahamu, ambaye hajasahau wema na uaminifu wake kwa bwana wangu. Yawe ameniongoza mimi mwenyewe moja kwa moja mpaka kwa jamaa ya bwana wangu!”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 24:27
31 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, Abramu akamwambia Loti: “Kusikuwe ugomvi kati yetu wala kati ya wachungaji wako na wachungaji wangu, kwa sababu sisi ni jamaa moja.


Atukuzwe Mungu Mukubwa, aliyetia waadui zako katika mikono yako!” Naye Abramu akamupa Melkisedeki sehemu moja ya kumi ya vitu vyote alivyokuwa navyo.


Naye akaomba: “Ee Yawe, Mungu wa bwana wangu Abrahamu, ninakuomba unisaidie leo na umutendee mema bwana wangu Abrahamu.


Yule mutu akakuwa anamwangalia kwa uangalifu bila kusema lolote, apate kufahamu kama Yawe amefanikisha safari yake au sivyo.


Uniapie kwamba utakwenda mpaka katika inchi yangu, kwa jamaa zangu, umutafutie mwana wangu Isaka muke.”


“Leo nilipofika kwenye kisima nikaomba: ‘Ee Yawe, Mungu wa bwana wangu Abrahamu, ninakuomba unisaidie leo katika safari yangu na umutendee Abrahamu bwana wangu mema.


Kisha nikainama na kumwabudu Yawe. Nikamutukuza Yawe, Mungu wa bwana wangu Abrahamu, ambaye ameniongoza moja kwa moja kwa binti wa ukoo wa bwana wangu kwa ajili ya mwana wake.


Kisha Yakobo akamwomba Mungu akisema: “Ee Mungu wa babu yangu Abrahamu, Mungu wa baba yangu Isaka! Ewe Yawe uliyeniambia nirudi katika inchi yangu kwa jamaa yangu, ukaniahidi kunitendea mema,


sistahili hata kidogo wema wote na uaminifu wote ulionitendea mimi mutumishi wako. Nilipovuka muto Yordani, sikukuwa na kitu isipokuwa fimbo; lakini sasa nina makundi haya mawili.


Tena akasema: “Semu abarikiwe na Yawe, Mungu wangu! Kanana akuwe mutumwa wake.


Halafu Ahimasi akamwambia mufalme kwa sauti kubwa: “Mambo yote ni sawa.” Akainama mbele ya mufalme, kwa heshima na kusema: “Yawe atukuzwe, Mungu wako, ambaye amekukomboa kutoka watu walioinua mikono yao juu yako, bwana wangu mufalme.”


Yawe ni muzuri! Wema wake unadumu milele, na uaminifu wake kwa vizazi vyote.


Anapanda juu akichukua wafungwa, anapokea zawadi kutoka kwa watu, hata kutoka kwa watu walioasi, Yawe apate kukaa huko.


Amekumbuka wema na uaminifu wake kwa Waisraeli. Pande zote za dunia zimeuona ushindi wa Mungu wetu.


Yetro akasema: “Atukuzwe Yawe ambaye amewaokoa toka katika mikono ya Wamisri na kutoka katika mukono wa mufalme wa Misri.


Siku moja, Musa alipokuwa mutu muzima, akawaendea Waebrania wenzake kwa kujionea taabu zao. Basi, akamwona Mumisri mumoja akimupiga Mwebrania, mumoja wa wandugu zake.


Kesho yake, Musa akatoka tena, akaona Waebrania wawili wakipigana. Basi, akamwuliza yule aliyekosa: “Kwa nini unamupiga mwenzako?”


Kisha Yawe akapita mbele ya Musa akitangaza tena: Yawe, Yawe, ni Mungu mwenye rehema na huruma, si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa wema na uaminifu.


Umutambue Mungu katika kila kitu unachofanya, naye atasawanisha njia zako.


Ninatembea katika njia ya haki; ninafuata sheria ya Mungu.


Utatuonyesha uaminifu na wema wako sisi wazao wa Abrahamu na wa Yakobo, kama ulivyowaahidi babu zetu tangu zamani.


“Asifiwe Bwana, Mungu wa Waisraeli, maana amewasaidia watu wake na kuwakomboa.


Sheria ya Mungu ilitolewa kwa njia ya Musa, lakini neema na ukweli vilikuja kwa njia ya Yesu Kristo.


Asifiwe Mungu, Baba ya Bwana wetu Yesu Kristo! Yeye ndiye aliyetupatia baraka za kiroho za kila namna kutoka katika eneo la mbingu kwa njia ya kuungana kwetu na Kristo.


Kwa Mufalme wa milele, asiyeweza kufa, asiyeonekana, Mungu peke yake, ikuwe heshima na utukufu milele na milele! Amina.


Halafu wanawake wa muji huo wakamwambia Naomi: “Atukuzwe Yawe ambaye hakukuacha leo bila kuwa na ndugu wa kukutunza! Mujukuu wako akuwe mwenye sifa kubwa katika Israeli!


Daudi akamwambia Abigaili: “Atukuzwe Yawe, Mungu wa Israeli, aliyekutuma leo kukutana nami.


Daudi aliposikia kwamba Nabali amekufa, alisema: “Atukuzwe Yawe ambaye amemulipiza kisasi Nabali kwa kunitukana, naye Yawe ameniepusha mimi mutumishi wake kutenda maovu. Yawe amemwazibu Nabali kwa uovu wake.” Kisha Daudi alituma watu kwa kumuchumbilia Abigaili akuwe muke wake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ