Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 24:26 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

26 Halafu yule mutu akainamisha kichwa chake, akamwabudu Yawe

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 24:26
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Akawaambia wale watumishi wake: “Mungoje hapa na huyu punda. Mimi na mwana wangu tutakwenda mpaka kule, tutamwabudu Mungu, kisha tutawarudilia.”


Kwetu kuna majani na malisho ya kutosha na pahali pa kulala kwa wageni.”


Kisha nikainama na kumwabudu Yawe. Nikamutukuza Yawe, Mungu wa bwana wangu Abrahamu, ambaye ameniongoza moja kwa moja kwa binti wa ukoo wa bwana wangu kwa ajili ya mwana wake.


Mutumishi wa Abrahamu aliposikia maneno hayo, akamwabudu Yawe.


Kisha, mufalme Daudi akawaambia wote waliokusanyika: “Mumusifu Yawe, Mungu wenu.” Na wote waliokusanyika wakamutukuza Yawe, Mungu wa babu zao, wakainama mbele yake na kumwabudu Yawe na kumutolea mufalme Daudi heshima.


Kisha mufalme Yosafati akainama uso mpaka chini pamoja na watu wote wa Yuda na wakaaji wa Yerusalema na kumwabudu Yawe.


Kisha mufalme Hezekia na viongozi wakawaambia Walawi wamusifu Yawe kwa nyimbo ambazo mufalme Daudi na nabii Asafu walizotunga. Basi, watu wote wakamutukuza Mungu kwa furaha, na kuinama uso mpaka chini.


Ezra akamushukuru Yawe, Mungu mukubwa na watu wote wakaitikia: “Amina! Amina!” nao wakiwa wakiinua mikono yao juu. Kisha wakamwabudu Mungu nazo nyuso zao zikigusa chini.


Maana Yawe ni mufalme; yeye anatawala mataifa.


Dunia yote inakuabudu; watu wote wanakuimbia sifa!”


Waadui zake wanaokaa katika jangwa wanyenyekee mbele yake, wapinzani wake walambule vumbi.


Mukuje tuiname chini na kumwabudu; tumupigie magoti Yawe, Muumba wetu!


ninyi mutawajibu: ‘Hii ni sadaka ya Pasaka kwa Yawe, kwa sababu alipita nyumba za Waisraeli katika inchi ya Misri. Aliwaua Wamisri, lakini sisi hakutuua.’ ” Waisraeli wakainamisha vichwa na kumwabudu Yawe.


Musa akainama uso mpaka chini haraka, akamwabudu Mungu.


Watu wakaamini. Na waliposikia kwamba Yawe amekuja kuwasaidia Waisraeli na kwamba ameyaona mateso yao, wote wakainamisha vichwa vyao na kumwabudu.


Nimwendee Yawe na kitu gani, nipate kumwabudu Mungu anayekuwa juu? Nimwendee na sadaka za kuteketezwa kwa moto, nimutolee mwana-ngombe wa mwaka mumoja?


kusudi kwa kuheshimu jina la Yesu, viumbe vyote vinavyokuwa katika mbingu, katika dunia na katika kuzimu, vipige magoti mbele yake,


Gideoni aliposikia masimulizi hayo ya ndoto na mafasirio yake, akamwabudu Mungu. Kisha akarudi kwenye kambi ya Waisraeli, akasema: “Musimame tuende, maana Yawe amelitia jeshi la Wamidiani katika mikono yenu.”


Kwa sababu hiyo, mimi ninamupa Yawe mutoto huyu; wakati wote atakapokuwa anaishi, ametolewa kwa Yawe.” Halafu, wakamwabudu Yawe pale.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ