Basi, binti nitakayemwambia atue mutungi wake wa maji anipatie maji nikunywe, naye akinipa mimi na kuwakunywesha ngamia wangu, akuwe ndiye uliyemuchagulia mutumishi wako Isaka. Jambo hilo litanionyesha kwamba umemutendea mema bwana wangu.”
Basi, akafanya haraka, akawamiminia ngamia maji ya mutungi wake katika birika, akakimbia kwenye kisima kuteka maji mengine na kuwakunywesha ngamia wake wote.