Basi, binti nitakayemwambia atue mutungi wake wa maji anipatie maji nikunywe, naye akinipa mimi na kuwakunywesha ngamia wangu, akuwe ndiye uliyemuchagulia mutumishi wako Isaka. Jambo hilo litanionyesha kwamba umemutendea mema bwana wangu.”
Naye akatua mutungi wake haraka toka juu ya bega lake, akasema: ‘Basi, kunywa bwana wangu. Nitatekea ngamia wako maji vilevile.’ Basi, mimi nikakunywa naye akawapa ngamia wangu maji vilevile.