Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 24:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Halafu yule mutumishi akaharakisha kukutana naye, akamwambia: “Tafazali, unipatie maji ya kunywa kutoka mutungi wako.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 24:17
10 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

“Mbele sijamaliza kuomba ndani ya moyo wangu, mara tu Rebeka akafika na mutungi wake wa maji juu ya bega, akateremuka kwenye kisima na kuteka maji. Nami nikamwambia: ‘Tafazali unipe maji ya kunywa.’


Basi, Elia akaondoka, akaenda Zerepata. Alipofika kwenye mulango wa muji, akamukuta mwanamuke mumoja mujane akiokota kuni. Elia akamwita mwanamuke huyo na kumwambia: “Uniletee maji nikunywe.”


Enyi wakaaji wa inchi ya Tema, muwape maji hao wenye kiu; muwapelekee chakula hao wakimbizi.


Wakati utakapofika ambapo waadui watauawa na minara yao kubomolewa, vijito vya maji vitatiririka kutoka kila mulima na kilima.


Hawatasikia tena njaa wala kuwa na kiu. Upepo wenye kuunguza wala jua havitawachoma, mimi niliyewahurumia nitawaongoza na kuwapeleka kwenye chemichemi za maji.


Halafu mwanamuke mumoja Musamaria akakuja kuteka maji. Na Yesu akamwambia: “Unipe maji ya kunywa.”


Basi yule mwanamuke Musamaria akamwambia Yesu: “Namna gani wewe Muyuda unaweza kuniomba mimi Musamaria maji ya kunywa?” (Wayuda hawakukuwa na ushirika na Wasamaria.)


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ