Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 24:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Basi, binti nitakayemwambia atue mutungi wake wa maji anipatie maji nikunywe, naye akinipa mimi na kuwakunywesha ngamia wangu, akuwe ndiye uliyemuchagulia mutumishi wako Isaka. Jambo hilo litanionyesha kwamba umemutendea mema bwana wangu.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 24:14
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini Abramu akamwambia: “Ee Yawe, nitajua namna gani kwamba nitarizi inchi hii?”


Niko hapa kando ya kisima ambapo wabinti za wenyeji wa muji wanakuja kuteka maji.


Mbele hajamaliza kuomba, mara moja Rebeka, binti ya Betueli mwana wa Milka, muke wa Nahori, ndugu ya Abrahamu, akafika akibeba mutungi wake kwenye bega.


Binti akamujibu: “Kunywa, ee bwana wangu.” Na palepale akatua mutungi wake, akiushikilia kusudi amukunyweshe.


Alipokwisha kumupatia maji, akamwambia: “Nitatekea ngamia wako maji vilevile, wakunywe mpaka watosheke.”


Niko hapa kando ya kisima. Binti atakayekuja kuteka maji ambaye nitamwomba anipatie maji kidogo ya kunywa kutoka mutungi wake,


naye akinipa na kuwatekea ngamia wangu maji, basi yule akuwe ndiye uliyemuchagua kuwa muke wa mwana wa bwana wangu.’


Yoabu akamwambia Amasa: “Habari gani ndugu yangu?” Yoabu akamushika Amasa kwenye kidevu kwa mukono wa kuume sawa vile anataka kumubusu.


Na mara moja mutakaposikia vishindo vya miguu kwenye vilele vya miforosadi hiyo, halafu ujipe moyo maana nitakuwa nimetoka kwa kukutangulia kuwapiga waaskari wa Wafilistini.”


Nyumba na mali ni urizi mutu anaopata kwa babu zake, lakini muke mwenye akili anatoka kwa Yawe.


Umwombe Yawe, Mungu wako, akupe kitambulisho; kikuwe ni kutoka chini kuzimu au juu mbinguni.


katika maombi yangu. Ninaomba kwamba Mungu akitaka, anifungulie njia ya kuwatembelea siku hizi.


Nao wakamwambia: “Tafazali utuulizie kwa Yawe kama tutafanikiwa katika safari yetu.”


Gideoni akamwambia: “Basi, ikiwa nimepata rehema kwako, unionyeshe kitambulisho kusudi nijue kwamba ni wewe kweli uliyezungumuza nami.


sasa ninaweka ngozi ya kondoo chini kwenye kiwanja cha kupepetea ngano. Ikiwa kutakuwa umande juu ya ngozi tu, na udongo unaouzunguka ikakuwa mukavu, basi, nitajua kwamba utawaokoa Waisraeli kwa mukono wangu kama ulivyosema.”


Ikiwa ataona hilo ni sawa, basi, ujue kwamba mambo yangu, mimi mutumishi wako, yako sawa. Kama sivyo, kusudi lake juu yangu ni baya.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ