Alipofika, alipigisha ngamia wake magoti kando ya kisima kilichokuwa inje ya muji. Ilikuwa magaribi wakati ambapo wanawake wanakwenda kwenye kisima kuteka maji.
Basi, binti nitakayemwambia atue mutungi wake wa maji anipatie maji nikunywe, naye akinipa mimi na kuwakunywesha ngamia wangu, akuwe ndiye uliyemuchagulia mutumishi wako Isaka. Jambo hilo litanionyesha kwamba umemutendea mema bwana wangu.”