Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 24:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Sasa Abrahamu alikuwa muzee wa miaka mingi, naye Yawe alikuwa amemubariki katika kila hali.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 24:1
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa, nitakubariki na kutukuza jina lako, nawe utakuwa baraka.


Wakati ule, Abramu alikuwa ametajirika sana. Alikuwa na makundi ya nyama, feza na zahabu.


Abrahamu na Sara walikuwa wazee sana, naye Sara hangeweza tena kuzaa.


Abrahamu alikuwa na umri wa miaka mia moja wakati mwana wake Isaka alipozaliwa.


Yawe amemubariki sana bwana wangu, naye amekuwa mutu mukubwa. Amemupa makundi ya kondoo na nyama wengi, feza na zahabu, watumishi wanaume na wanawake, ngamia na punda!


Isaka alipokuwa na umri wa miaka makumi ine akamwoa Rebeka, binti ya Betueli, Musuria wa Padani-Aramu. Rebeka alikuwa dada ya Labani.


Mwaka ule Isaka akapanda mbegu katika inchi ile, akavuna mara mia zaidi, maana Yawe alimubariki,


Mungu wa baba yako atakusaidia, Mungu Mwenye Nguvu atakubariki, upate baraka za mvua toka juu mbinguni, baraka za maji ya vilindi vinavyokuwa chini, baraka za uzazi wa wamama na nyama.


Wakati mufalme Daudi alipokuwa muzee sana, watumishi wake walimufunika kwa mablanketi, lakini, hata hivyo, hakuweza kupata joto.


Baraka za Yawe ndizo zinazoleta utajiri. Juhudi za mutu haziongezi kitu.


Mukumbuke Abrahamu babu yenu, na Sara aliyewazaa ninyi. Abrahamu alikuwa hana mutoto wakati nilipomwita, lakini nilimubariki na kumufanya kuwa na wengi.


Lakini ninyi mushugulikie kwanza Ufalme wa Mungu na kufuata haki mbele yake, naye atawaongezea vitu vile vyote.


Lakini hawakukuwa na mutoto, kwa maana Elizabeti alikuwa tasa, tena wote wawili walikuwa wazee sana.


Kufuatana na hiyo, Mungu atawabariki wote wanaoamini sawa vile alivyomubariki Abrahamu, mwenye imani.


Asifiwe Mungu, Baba ya Bwana wetu Yesu Kristo! Yeye ndiye aliyetupatia baraka za kiroho za kila namna kutoka katika eneo la mbingu kwa njia ya kuungana kwetu na Kristo.


Mazoezi ya mwili yana mafaa kidogo, lakini kushikamana na ibada kuna mafaa katika mambo yote, kwa maana kunatupatia ahadi ya kuishi kwa wakati huu wa sasa na kwa wakati utakaokuja.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ