Yakobo akamujibu: “Umri niliojaliwa kama musafiri ni miaka mia moja na makumi tatu. Miaka hiyo imekuwa michache na iliyojaa mateso, tena haijafikia hesabu ya miaka wazee wangu waliyoishi kama wasafiri.”
kule Makipela, upande wa mashariki wa Mamure, katika inchi ya Kanana. Abrahamu alinunua pango na shamba hilo kwa Efuroni, Muhiti, likuwe lake la kuzikia.
wakamupeleka mpaka inchi ya Kanana, wakamuzika katika pango lililokuwa katika shamba kule Makipela, upande wa mashariki wa Mamure. Pango pamoja na shamba lile Abrahamu alikuwa amelinunua kwa Efuroni Muhiti, kusudi pakuwe pahali pake pa kuzikia.
Sisi tuko wageni mbele yako, na wasafiri kama vile babu zetu walivyokuwa wote. Siku zetu katika dunia ni kama kivuli kinachopita, hapa hakuna tumaini la kukaa.
watu wanaogopa mupando na kutishwa katika njia, muti wa lozi unachanua maua yake meupe, mapanzi hayawezi kuruka, hakuna hamu tena, mwanadamu anaelekea kwenye makao yake ya milele, waombolezaji wanasambaa katika njia,
Mutu akiweza kuzaa watoto mia moja, na akiishi maisha marefu, lakini kama mutu huyo hafurahii maisha yake, wala hafanyiwi mazishi, basi ninasema mutoto aliyezaliwa amekufa ni afazali kuliko mutu yule.
Kule Mungu hakumupa Abrahamu hata sehemu ndogo ya shamba inayokuwa kama kikanyagio cha muguu kuwa urizi wake, lakini alimwahidi kwamba atamupa inchi hii kuwa urizi wake na wa wazao wake watakaoishi nyuma yake. Wakati ule, alikuwa hana mutoto.
Kwa njia ya imani, aliishi kama vile mugeni katika inchi ile Mungu aliyomwahidi. Yeye alikuwa akiishi katika hema kama vile Isaka na Yakobo walivyoishi. Wao vilevile walishiriki pamoja naye ahadi ile ile ya Mungu.