Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 23:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Alikufia kule Kiriati-Arba, ni kusema Hebroni, katika inchi ya Kanana. Abrahamu akaomboleza na kumufanyia Sara muke wake kilio.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 23:2
36 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kwa hiyo, Abramu akaongoa hema, akakwenda kukaa karibu na mielo ya Mamure kule Hebroni. Kule akajengea Yawe mazabahu.


Sara aliishi miaka mia moja makumi mbili na saba. Hiyo ndiyo iliyokuwa miaka ya maisha ya Sara.


Nyuma ya hayo, Abrahamu akamuzika Sara muke wake katika pango lile lililokuwa mule katika shamba la Makipela, upande wa mashariki ya Mamure, ni kusema Hebroni, katika inchi ya Kanana.


Basi, Isaka akamutwaa Rebeka ndani ya hema iliyokuwa ya mama yake Sara, naye akakuwa muke wake. Isaka akamupenda Rebeka na kupata kufarijika nyuma ya kifo cha mama yake.


Basi, Esau akamuchukia Yakobo kwa sababu ya baraka aliyokuwa amepewa na baba yake. Esau akawaza: “Siku za kilio cha baba zitakapokwisha, ndipo nitakapomwua ndugu yangu Yakobo.”


Yakobo akaondoka akakwenda Mamure kwa baba yake Isaka, kule Kiriati-Arba ni kusema Hebroni, pahali ambapo Abrahamu na Isaka walikaa kama wageni.


Baba yake akamwambia: “Kwenda uwaangalie wandugu zako na nyama kama wako salama, kisha uniletee habari.” Basi, Yakobo akamutuma Yosefu kutoka bonde la Hebroni. Yosefu alipokaribia Sekemu,


Yosefu akamukumbatia baba yake akilia na kumubusu.


Walipofika katika uwanja wa kupepetea ngano wa Atadi, ngambo ya muto Yordani, waliomboleza kwa huzuni kubwa, naye Yosefu akamufanyia baba yake marehemu kilio cha siku saba.


Wakaomboleza, wakalia na kufunga kula mpaka magaribi kwa ajili ya Saulo, Yonatani mwana wake, na inchi ya Waisraeli, watu wa Yawe, kwa maana wengi kati yao waliuawa katika vita.


Daudi aliimba maombolezo haya kwa ajili ya Saulo na mwana wake Yonatani.


Daudi alikuwa mufalme wa kabila la Yuda kwa muda wa miaka saba na nusu, makao yake yalikuwa kule Hebroni.


Basi, wazee wote wa Waisraeli wakamwendea mufalme Daudi kule Hebroni. Naye akafanya agano nao mbele ya Yawe, halafu wakamupakaa Daudi mafuta akuwe mufalme wa Israeli.


Kule Hebroni, alitawala watu wa Yuda kwa muda wa miaka saba na miezi sita, na kule Yerusalema alitawala watu wa Israeli pamoja na Yuda kwa muda wa miaka makumi tatu na mitatu.


Katika kabila la Isakari walipewa: Kedesi pamoja na mashamba yake ya malisho, Deberati pamoja na mashamba yake ya malisho,


Nabii Yeremia vilevile akatunga shairi la maombolezo kwa ajili ya kifo chake; nao waimbaji wote, wanaume na wanawake, wanamutaja Yosia katika maombolezo yao, mpaka leo. Wakakusudia kuwa wanafanya maombolezo haya katika Israeli; angalia nayo yameandikwa katika Maombolezo.


Watu wengine walikaa katika miji karibu na mashamba yao. Watu wamoja wa kabila la Yuda walikaa Kiriati-Arba, Diboni na Yekabuseli pamoja na vijiji vilivyoizunguka.


Musimulilie yule aliyekufa, musiomboleze kwa ajili yake. Lakini mumulilie kwa uchungu yule anayekwenda mbali kwa sababu hatarudi tena kuiona inchi yake.


Kwa hiyo, Yawe anasema hivi juu ya Yoyakimu mwana wa Yosia, mufalme wa Yuda: Wakati atakapokufa, hakuna atakayeomboleza juu yake, akisema: Yowe, ndugu yangu! Yowe, dada yangu! Wala hakuna atakayemulilia, akisema: Yowe, bwana wetu! Yowe, muheshimiwa wetu!


Wakakwenda mpaka Negebu wakapita mpaka muji wa Hebroni. Humo wakawakuta Waahimani, Wasesai na Watalmai, wazao wa Anaki. (Muji wa Hebroni ulikuwa umejengwa miaka saba mbele ya muji wa Soani unaokuwa katika inchi ya Misri).


Waisraeli walipoona kwamba Haruni amekufa, wakafanya kilio cha siku makumi tatu.


Wakati wale Wayuda waliokuwa ndani ya nyumba pamoja na Maria kwa kumufariji walipomwona akisimama upesi na kutoka, wakamufuata. Walizani kama anakwenda kulia kwenye kaburi.


Watu wenye kuogopa Mungu wakamuzika Stefano na kumufanyia kilio kikubwa.


Waisraeli wakaomboleza kifo chake kwa muda wa siku makumi tatu kwenye inchi ya bonde la Moabu. Kisha siku za kilio na maombolezo ya kifo chake zikaisha.


Waliuteka muji huo na mufalme wake pamoja na miji mingine yote iliyouzunguka na kuwaangamiza wote waliokuwa ndani yao bila kuacha hata mutu mumoja. Waliutendea muji huo kama walivyoutendea muji wa Hebroni na muji wa Libuna na wafalme wao.


Kalebu mwana wa Yefune, alipewa sehemu ya inchi ya Yuda kama vile Yawe alivyomwamuru Yoshua. Alipewa Kiriati-Arba au muji wa Arba ambaye alikuwa babu wa Anaki. Muji huo sasa unaitwa Hebroni.


Basi, kwa ajili hiyo wakaitenga miji ya Kedesi katika Galilaya kwenye milima ya Nafutali, Sekemu katika milima ya Efuraimu na Kiriati-Arba, ni kusema Hebroni, katika inchi ya milima ya Yuda.


Wakapewa Kiriati-Arba, ni kusema Hebroni (Arba alikuwa baba ya Anaki), katika milima ya Yuda, pamoja na mbuga zilizoizunguka.


Waliwashambulia vilevile Wakanana walioishi katika muji wa Hebroni ambao zamani uliitwa Kiriati-Arba, wakashinda makabila ya Sesai, Ahimani na Talmayi.


Wewe, haujui kwamba wakati mwana wa Yese angali anaishi katika dunia, wewe hautaweza kuwa na uhakika wa kuwa mufalme wa inchi hii? Sasa hivi kwenda umulete hapa kwangu, kwa sababu anapaswa kuuawa.”


Sasa, Samweli akakufa. Nao Waisraeli wote wakakusanyika kwa kumwomboleza. Wakamuzika kwenye nyumba yake kule Rama. Kisha Daudi akaenda zake kwenye jangwa za Parani.


Wakati ule, Samweli alikuwa amekwisha kufa, na Waisraeli wote walikuwa wamekwisha kumwombolezea na kumuzika katika muji wake Rama. Saulo alikuwa amewafukuza kutoka katika inchi wenye kutabiri na wachawi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ