Mutu yeyote atakayeua mutu, atahukumiwa kifo kutokana na ushuhuda wa washuhuda wawili au zaidi; mutu yeyote hawezi kuhukumiwa kifo kutokana na ushuhuda wa mutu mumoja.
“Ushuhuda wa mutu mumoja hautoshi kwa kuhukumu mutu juu ya kosa lolote au uovu juu ya kosa lolote alilofanya. Ni ushuhuda wa watu wawili au watatu tu ndio utakaohakishwa.
Boazi akakwenda kwa nafasi ya kufanyia mukutano kule kwenye mulango wa muji, akaikaa chini. Kisha yule ndugu ya Elimeleki ambaye Boazi alikuwa amemutaja, akapita karibu na pale. Boazi akamwita, akasema: “Kuja, uikae hapa ndugu.” Basi yule mutu akakuja na kuikaa pale.
Basi wazee waliokuwa kwenye mulango na watu wote waliokuwa pale wakajibu: “Ndiyo, sisi ni washuhuda. Yawe amufanye muke wako akuwe kama Rakeli na Lea, ambao wote wawili waliijenga nyumba ya Israeli. Nawe upate kustawi katika jamaa ya Efurata, ukuwe na sifa katika Betelehemu.
Basi mimi nimeona afazali nikujulishe habari hii. Sasa ikiwa unalitaka shamba hili, ulinunue mbele ya wazee wa watu wangu. Ikiwa unalitaka au haulitaki sema basi kwa sababu nafasi ya kwanza ya kulikomboa ni yako, na yangu ni ya pili.” Naye akasema: “Mimi nitalikomboa.”
Halafu Boazi akawaambia wazee na watu waliokuwa pale: “Leo ninyi ni washuhuda wangu. Mumeona kwamba nimenunua kutoka kwa Naomi, vyote vilivyokuwa vya Elimeleki, na vya Kiliona na Malona.