Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 22:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Abrahamu akamujibu: “Mwana wangu, Mungu mwenyewe atatujalia mwana-kondoo wa sadaka ya kuteketezwa.” Basi, wakaendelea na safari yao.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 22:8
14 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kuna jambo lolote lisilowezekana kwa Yawe? Nitakurudilia wakati uliopangwa, kwa wakati kama huu katika mwaka, na Sara atakuwa na mutoto mwanaume.”


Kwa hiyo, Abrahamu akapaita pahali pale: “Yawe anajalia,” kama inavyosemwa hata leo: “Kwa mulima wa Yawe, watu wanajaliwa.”


Isaka akamwuliza baba yake: “Baba, tuko na moto na kuni. Lakini mwana-kondoo wa sadaka ya kuteketezwa yuko wapi?”


Walipofika pahali ambapo Mungu alipomwagiza, Abrahamu akajenga mazabahu na kupanga kuni juu yake. Kisha akamufunga Isaka mwana wake na kumulalisha juu ya kuni kwenye mazabahu.


Kisha Elia akamwambia Elisha: “Tafazali ubakie hapa. Yawe amenituma niende Yordani.” Lakini Elisha akasema: “Kama vile Yawe anavyoishi na kama vile unavyoishi, sitakuacha.” Basi, wakaenda pamoja.


Amazia akamwuliza yule mutu wa Mungu: “Tutafanya nini na feza yote ambayo nimekwisha wapa waaskari wa Israeli?” Naye akamujibu: “Yawe anaweza kukupa zaidi ya hiyo.”


Yesu akawaangalia na kuwaambia: “Jambo hilo haliwezi kutendeka kwa uwezo wa mwanadamu, lakini kwa uwezo wa Mungu, yote yanawezekana.”


Kesho yake Yoane akamwona Yesu akikuja kwake, akasema: “Angalia Mwana-Kondoo wa Mungu anayeondoa zambi ya dunia!


Wakati alipomwona Yesu akipita, akasema: “Angalia Mwana-Kondoo wa Mungu.”


Wakaaji wote wa dunia watamwabudu, ndio wale wote ambao tangia kuumbwa kwa dunia, majina yao hayakuandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo aliyechinjwa.


Nao waliimba hivi kwa sauti kubwa: “Mwana-Kondoo aliyeuawa anastahili kupokea uwezo, utajiri, hekima na nguvu, heshima, utukufu na sifa!”


Halafu nikaona Mwana-Kondoo akisimama katikati ya kiti cha kifalme chenye kuzungukwa na vile viumbe vine vya ajabu na wale wazee, naye alionekana kama amechinjwa. Alikuwa na pembe saba na macho saba; ndizo roho saba za Mungu zilizotumwa katika dunia yote.


Nami nikamujibu: “Bwana wangu wewe ndiwe unayejua.” Naye akaniambia: “Hawa ndio wanaotoka katika mateso makubwa. Wamesafisha kanzu zao na kuzifanya kuwa nyeupe katika damu ya Mwana-Kondoo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ