Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 22:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Kwa siku ya tatu, Abrahamu aliinua macho akaona pahali pale kwa mbali.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 22:4
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, kesho yake, Abrahamu akaamuka asubui mapema, akatandika punda wake, akawatwaa watumishi wake wawili pamoja na Isaka mwana wake. Akatayarisha kuni kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa kwa moto, kisha akaanza safari kuelekea pahali alipoambiwa na Mungu.


Akawaambia wale watumishi wake: “Mungoje hapa na huyu punda. Mimi na mwana wangu tutakwenda mpaka kule, tutamwabudu Mungu, kisha tutawarudilia.”


“Rudi umwambie Hezekia, mukubwa wa watu wa Yawe, na kumwambia: Mimi, Yawe, Mungu wa babu yako Daudi, nimesikia ombi lako na nimeona machozi yako. Nitakuponyesha na nyuma ya siku tatu utaenda katika nyumba ya Yawe.


Kisha siku tatu ya kufunga kwake, Esteri akavaa nguo zake za kimalkia, akaenda kusimama katika kiwanja cha ndani cha nyumba ya mufalme, kuelekea chumba cha mufalme. Mufalme alikuwa mule ndani akiikaa katika kiti chake cha kifalme, kuelekea mulango wa nyumba ya mufalme.


Kisha, Musa akawaongoza Waisraeli kutoka bahari Nyekundu, wakaenda mpaka kwenye jangwa la Suri. Wakasafiri kwa muda wa siku tatu katika jangwa bila kuona maji yoyote.


wakuwe tayari kwa kesho kutwa, maana siku hiyo ya tatu mimi Yawe nitashuka juu ya mulima Sinai mbele ya watu wote.


Kisha akawaambia watu wote: “Kesho kutwa mukuwe tayari na mwanaume yeyote asimukaribie mwanamuke.”


Musa na Haruni wakamwambia: “Mungu wa Waebrania amekutana nasi. Tunakusihi utuache tujiendee katika jangwa mwendo wa siku tatu tutoe sadaka kwa Yawe, Mungu wetu. Kama sivyo, yeye atatuua kwa ugonjwa mukali au kwa upanga.”


Nyuma ya siku mbili atatupatia tena uzima. Nyuma ya siku tatu atatufufua kusudi tuweze kuishi pamoja naye.


Lakini nyama yoyote ya sadaka hiyo inayobaki mpaka kwa siku ya tatu itateketezwa.


Basi, watu wakasafiri toka Sinai, mulima wa Yawe, mwendo wa siku tatu. Sanduku la Agano la Yawe liliwatangulia mwendo wa siku tatu, kwa kuwatafutia pahali pa kupigia kambi.


Siku ya tatu na ya saba mutu huyo atajitakasa kwa yale maji ya utakaso, naye atakuwa safi. Lakini akiacha kujitakasa katika siku ya tatu na ya saba, mutu huyo atabaki muchafu.


Katika siku ya tatu na ya saba, mutu anayekuwa safi atamunyunyizia mutu anayekuwa muchafu maji hayo; hivyo katika siku ya saba, atamutakasa mutu huyo anayekuwa muchafu, naye atafua nguo zake na kuoga, na magaribi atakuwa safi.


Wote wale wanaokuwa kati yenu ambao wameua mutu au kugusa maiti wanapaswa kukaa inje ya kambi kwa muda wa siku saba; mujitakase pamoja na mateka wenu katika siku ya tatu na ya saba.


nao watamwua, lakini kwa siku ya tatu kisha kufa kwake, atafufuka.” Halafu wanafunzi wakahuzunika sana.


Yesu akawajibu: “Mwende kumwambia yule mbweha: ‘Leo na kesho nitafukuza pepo na kuponyesha wagonjwa, na kesho kutwa nitamaliza kazi yangu.’


Alizikwa na kufufuliwa kwa siku ya tatu kisha kufa kwake kama vile Maandiko Matakatifu yanavyosema.


“Mupite katika kambi na kuwaamuru watu watayarishe chakula, kwa sababu kisha siku tatu mutavuka muto Yordani, kwenda kuirizi inchi ambayo Yawe, Mungu wenu, anawapa ikuwe mali yenu.”


Kisha, Daudi akaenda upande wa pili wa bonde hilo, akasimama juu kwenye mulima mbali na kundi la Saulo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ