Kisha, Sarai akamupa Abramu Hagari, mujakazi wake Mumisri, akuwe muke wake. Haya yalitokea nyuma ya Abramu kukaa katika inchi ya Kanana kwa muda wa miaka kumi.
Lakini akawapa wana wa habara zake zawadi. Na wakati alipokuwa bado muzima, akawapeleka katika inchi ya upande wa mashariki, mbali na mwana wake Isaka.
Kalebu alikuwa na habara mwingine jina lake Maka. Huyu akamuzalia wana hawa: Seberi, Tirana, Safu aliyekuwa mwanzilishi wa muji wa Madimana, na Sewa aliyekuwa mwanzilishi wa muji wa Makibena na Gibea. Kalebu alikuwa vilevile na binti, jina lake Akisa.