Kisha, yule mutumishi akatwaa ngamia kumi wa bwana wake akaondoka akiwa na zawadi nzuri za kila aina. Akasafiri kwenda katika muji Nahori alimokaa, katika inchi ya Mesopotamia.
Mbele hajamaliza kuomba, mara moja Rebeka, binti ya Betueli mwana wa Milka, muke wa Nahori, ndugu ya Abrahamu, akafika akibeba mutungi wake kwenye bega.