Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Mwanzo 22:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Mungu akamwambia: “Umutwae mwana wako, Isaka, mwana wako wa pekee unayemupenda, uende mpaka inchi ya Moria, umutoe kuwa sadaka ya kuteketezwa kwa moto juu ya mulima nitakaokuonyesha.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Mwanzo 22:2
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mungu akamujibu: “Hapana. Muke wako Sara atakuzalia mutoto mwanaume, nawe utamwita Isaka. Nitaimarisha agano langu kwake na wazao wake, kuwa agano la milele.


Lakini Mungu akamwambia Abrahamu: “Usihuzunike kwa sababu ya mutoto huyu, wala huyo mujakazi wako. Jambo lolote Sara atakalokuambia ulifanye. Maana ni kwa njia ya Isaka utapata wazao watakaoitwa wako.


Abrahamu akamupa huyo mwana wake ambaye Sara alimuzalia jina la Isaka.


Malaika akamwambia: “Usinyooshe mukono wako juu ya kijana wala usimufanyie jambo lolote! Sasa ninajua kwamba unamwogopa Mungu, maana haukuninyima hata mwana wako wa pekee.”


akamwambia: “Yawe anasema hivi: Nimeapa kwa nafsi yangu mwenyewe kwamba kwa sababu umefanya hivi, wala haukuninyima mwana wako wa pekee,


Basi, kesho yake, Abrahamu akaamuka asubui mapema, akatandika punda wake, akawatwaa watumishi wake wawili pamoja na Isaka mwana wake. Akatayarisha kuni kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa kwa moto, kisha akaanza safari kuelekea pahali alipoambiwa na Mungu.


Walipofika pahali ambapo Mungu alipomwagiza, Abrahamu akajenga mazabahu na kupanga kuni juu yake. Kisha akamufunga Isaka mwana wake na kumulalisha juu ya kuni kwenye mazabahu.


Noa akamujengea Yawe mazabahu, akatwaa mumoja katika kila aina ya nyama wanaohesabiwa kuwa safi na ndege anayehesabiwa kuwa safi, akamutolea Mungu sadaka za kuteketezwa kwa moto juu ya mazabahu.


Hapo akamutwaa mwana wake wa kwanza ambaye angekuwa mufalme kwa pahali pake, akamutoa kuwa sadaka ya kuteketezwa juu ya ukuta wa muji. Watu wa Israeli walipoona hayo, wakachukizwa sana. Wakauacha muji ule na kurudia katika inchi yao.


Kisha Solomono akaanza kujenga nyumba ya Yawe katika Yerusalema juu ya mulima Moria ambapo Yawe alimutokea Daudi baba yake, pahali ambapo Daudi alikuwa amepachagua, kwenye kiwanja cha kupepetea ngano cha Ornani Muyebusi.


Yawe atapendezwa nikimutolea maelfu ya kondoo dume, au mito elfu na elfu ya mafuta? Nimutolee muzaliwa wangu wa kwanza kwa ajili ya kosa langu, mutoto wangu wa kwanza kwa ajili ya zambi yangu?


Kwa maana Mungu alipenda sana ulimwengu hata kumutoa Mwana wake wa pekee, kusudi kila mutu anayemwamini asipotee, lakini apate uzima wa milele.


Lakini Mungu ameonyesha wazi upendo wake kwetu ni wapata gani, kwa maana tulipokuwa tungali wenye zambi, Kristo alikufa kwa ajili yetu.


Yeye hakumwacha Mwana wake wa pekee, lakini alimutoa kwa ajili yetu sisi wote. Namna gani atakosa kutupatia vilevile vitu vyote kwa njia ya mwana wake?


Kwa njia ya imani, Abrahamu alimutoa Isaka kama vile sadaka wakati Mungu alipopima imani yake. Abrahamu alikubali kumutoa mwana wake wa pekee, ingawa ni yeye ndiye aliyekuwa amepewa ahadi na Mungu.


basi, yeyote atakayetoka inje kutoka katika nyumba yangu kuja kunipokea nitakapokuwa ninarudi nyuma ya kuwashinda Waamoni, huyo atakuwa wako wewe Yawe. Nitakutolea kama sadaka ya kuteketezwa.”


Nyuma ya miezi miwili akarudi kwao. Kisha baba yake akamutendea kulingana na kiapo chake. Binti huyo hakukuwa amemujua mwanaume yeyote. Basi, tangu wakati ule kukakuwa desturi hii katika Israeli:


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ